Mwamko Mdogo Wa Wazazi Kuchangia Vyakula Shuleni , Chanzo Cha Utoro Kwa Wanafunzi Wa Darasa la kwanza

wanafunzi awali wakiripoti shule
 

Na Baraka Lusajo – Rukwa 

Imeelezwa kuwa ukosefu wa sheria inayo weza kuwalazimisha wazazi na walezi kuchangia vyakula mashuleni  imekuwa chanzo cha wanafunzi  wengi wa madarasa ya kwanza na awali mkoani Rukwa  kuwa watoro na wengine kuacha shule kisha kutumikishwa kwenye shughuli za uvuvi na ufugaji.

Hayo yanajiri siku  chache baada  shule nyingi  za msingi mkoani humo kushindwa kutoa vyakula shuleni  ,ambapo hadi kufikia machi 2024 shule 106 za msingi kati 338 mkoani humo zilishindwa kutoa chakula huku chanzo ikidaiwa ni uwepo wa mwamko mdogo wazazi na walezi wa uchangia vyakula shuleni  husani kwa wanafunzi wa awali na darasa la kwanza.

 kushoto ni mwenyekiti wa CWT koani Rukwa

 Mwenyekiti wa chama cha walimu (CWT) mkoani Rukwa Doseph Ndalama,  Alisema serikali haina budi kuanza kufikiria kuupeleka bungeni muswada wa sheria utakao walazimisha wazazi na walezi kuchangia vyakula shuleni ili kupunguza utoro kwa wanafunzi na kubainisha kuwa hiyo itasaidia wanafunzi kupenda shule  na kusisitiza kuwa zoezi la utoaji  chakula shuleni linapaswa kuwa la lazima.

‘’ili tupate watoto watakao kuwa bora kitaalumu ni lazima wazazi tuwahimize kuchangia vyakula shule na hili lianzie elimu ya awali ambako ndiko  chimbuko la mtoto la kumjengea uwezo kitaaluma linako anzia.’’ Alisema Ndala.

Kwa upande wake mbunge wa Viti Maalumu mkoani humo Bupe Mwakang’ata ,Alisema wazazi na walezi wanawajibu wa kulichukua swala la utoaji vyakula  mashuleni  kama kipaumbele cha kwanza ili kuinua ufaulu na taalamu shuleni na kubainisha kuwa wanafunzi wengi  wa darasa la kwanza wamekuwa watoro na kujihusisha na shughuli za ufugaji na uvuvi.

Alisema wao kama wabunge wa mkoa watahakikisha wanalichukulia swala hilo kwa uzito ikiwezekana kuongea na ofisi ya mkuu wa mkoa  ili kutungwa sheria ndogo  zitakazo wawajibisha wazazi na walezi wanashindwa kuwapeleka watoto wao shuleni kisha kuwatumikisha kwenye shughuli za uzalishaji mali ikiwemo ufugaji na uvuvi.

Kwa upande Francis Nkyanduale, alisema  Tanzania ni nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika mashariki  hivyo kuwepo kwa mazingira rafiki ya kisera kumepelekea ongezeko la ufundishaji kuongezeka mwaka hadi mwaka na kwamba ili kufikia malengo zaidi serikali haina budi kuweka utarabu mzuri utakao wezesha wazazi wanaoshindwa kuwapeleka watoto shuleni kuchukuliwa hatua za kisheria ikiwemo kufikishwa mahakamani.

Kwa mujibu wa afisa taalumu mkoani Rukwa Matinda Mwinuka akiwa  ofisini, alisema serikali ya mkoa kwa kushirikiana na walimu  wameanza kukaa vikao  na kufikia  hitimisho la  wazazi na walezi  kuanza kuchangia vyakula mashul

  katika picha ni afisa elimu taaluma mkoa wa Rukwa 

eni na kwamba kwa sasa asilimia 72 ya watoto  wa awali na darasa  la kwanza wameanza kupata chakula  wakiwa shuleni.

‘’ kwa kushirikiana na walimu na viongozi wa serikali za vijiji na kata tumetoa elimu kwa wazazi na walezi na wameridhia kuanza kuchangia vyakula shule kwa kutoa debe moja la mahindi , sado moja ya maharangwe na fedha shilingi elfu kumi kwa kila mwezi .alisema Mwinuka.

Awali akiongea wakati wa tathimini ya utekelezaji wa mpango wa program jumuishji ya  taifa ya malezi makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto  kwa ngazi ya mkoa, katibu tawala mkoani Rukwa Gerald Kusaya , aliwaagiza wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo kutunga sheria ndogo zitakazo walazimisha wazazi na walezi kuchangia vyakula mashuleni na kusisitiza  shule zote kuweka mpango endelevu watoto wa awali kupata chakula.

Licha ya hilo alitishia kuwandikia barua za kujieleza wakurugenzi ambao watashindwa kutenga bajeti ya fedha shilingi elfu moja kwa ajili ya uendeshaji wa maswala ya lishe.

Makongoro Nyerere ni Mkuu wa mkoa wa Rukwa ambapo akiwa ofisni kwake alikiri uwepo wa utoro mashuleni na kuelezea hali ya uandikishaji wa wanafunzi wa awali na darasa la kwanza  kwa mwaka 2024 na kubainisha kuwa mkoa ulifanikiwa kuandikisha watoto wapato elfu thelathini. Ambapo ulilenga kuandikisha Wanafunzi 57,006 kati yao jinsia ya kiume wakiwa 27,885 na jinsia ya kike wakiwa 29,121) hadi kufikia tarehe 04 Januari, 2024 Wanafunzi 24,033 wa darasa la awali sawa na asilimia 42.1 walikuwa wameandikishwa kuanza darasa la awali.

‘’ Kwa upande wa darasa la kwanza Mkoa ulilenga kuandikisha W



anafunzi 51,347 kati yao jinsia ya kiume wakiwa 25,254 na jinsia ya kike wakiwa 26,093) ambapo mpaka tarehe 04 Januari, 2024 Jumla ya Wanafunzi 30,922 walikuwa wameandikishwa kujiunga na darasa la kwanza sawa na asilimia 60.2’’. alisema Makongoro.

Aidha alisesema kwa upande wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu jumla ya wanafunzi wa darasa la awali 167 kati yao jinsia ya kiume wakiwa 69 na wakike 98) waliandikishwa na kwa upande wa darasa la kwanza Wanafunzi wenye mahitaji maalumu jumla ya wanafunzi 91, waliandikishwa.

Kaimu afisa elimu msingi wilayani Kalambo akiwa ofisini kwake Kanuti Mbawala ,alisema hadi kufikia tarehe 18/1/2024 halmashauri ilikuwa na maoteo ya kuandikisha wanafunzi wa darasa la kwanza 10,901 kati yao wavulana wakiwa 5,382 na wasichana 5,519 na kwamba hadi kufikia tarehe 18/1/2-26 halmashauri ilifanikiwa kuandikisha wanafunzi 9,492 kati yao wavulana wakiwa  4,771 na wasichana 4,721.

‘’Pia halmashauri tumefanikiwa kuandikisha wanafunzi wenye mahitaji maalumu 4 kati yao wavulana wakiwa ni 1 na wasichana wakiwa 3, ambapo hadi kufikia sasa halmashauri imefanikiwa kufikia asilimia 87 ya uandikishaji.’’alisema Kanuti.

 Alisema Kwa upande wa wanafunzi wenye mahitaji maalumu jumla ya wanafunzi wa darasa la awali 167 kati yao jiansia ya kiume wakiwa 69 na wakike 98) waliandikishwa na kwa upande wa darasa la kwanza kwa wanafunzi wenye mahitaji maalum jumla ya wanafunzi 91, waliandikishwa na kuanza masomo.

Mkuu wa wilaya ya Kalambo Lazaro  Komba  akiwa ofisni kwake, alisema wilaya ya Kalambo imefanikiwa kukamilisha vyumba 39 vya madarasa  vyenye thamani ya shilingi billion 1.3  kwa ajili ya wanafunzi wa awali na kubainisha kuwa lengo la serikali ni kuhakikisha wanafunzi wote wanaripoti shule na kuendelea na masomo.

 Mkuu wa wilaya Nkasi  Peter Lijualikali akiwa ofisini kwake, alisema wanafunzi wote waliokuwa wameandikishwa wameripoti shule na kundelea na masomo na kuipongeza serikali kwa kukamilisha vyumba vya madarasa ambavyo vimewezesha wanafunzi wengi zaidi kuanza masomo kwa mwaka 2024.

Baadhi ya wakazi wa mkoa wa Rukwa akiwemo Brown Mtawa ambao licha ya kuipongeza serikli kwa kuwekeza fedha nyingi kwenye ujenzi vyumba vya madarasa ,waliishauri serikali kuona uwezekano wa  kuongeza idadi ya walimu wa shule za msingi ili kuendana na ongezeko la madarasa na wanafunzi wanao ripoti shule.

Awali akiongea ofisini kwake mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Kalambo shafi Mpenda ,alisema  pamoja na mambo mengine halmashauri kushirikiana na TAMISEMI imeanzisha mpango wezeshi  wa kuwatambua wanafunzi wa shule za msingi wasio jua kusoma ,kuandika na kuhesabu  kutokana na wanafunzi  2,470  wa darasa la kwanza na la pili kushindwa kumudu KKK.

Alisema  kwa mwaka 2023 wanafunzi  1,546  wa darasa la kwanza sawa na asilimia 12 walionekana na kushindwa kumudu kusoma , kuandika na kuhesabu huku wanafunzi 10,527  waliweza   kumudu KKK  yaani kusoma kuandika na kuhesabu kupitia program maalumu ya kuhakikisha wanafunzi wote wa darasa la kwanza wanamudu KKK.

Amesema licha ya hilo wanafunzi 10,667  kati yao wanafunzi 11,591 wa darasa la pili  walibainika kumudu kkk huku wanafunzi 924  sawa na asilimia 8 wakishindwa kumudu KKK na kuongeza  kuwa  jumla  ya wanafunzi 8,976  wa darasa la tatu sawa na asilimia 90 walibainika kumudu Lugha ya kingereza huku wanafunzi 976 sawa na asilimia 10 walishindwa kumudu lugha ya kingereza.

Hata hivyo baadhi ya wadau wa elimu kutoka taasisi zisizo kuwa za kiserikali akiwemo  Mosses Mwangata,  waliishauri serikali  kuona uwezekano wa kupeleka muswada bungeni  ili kutungwa sheria itakayo walazimisha wazazi na walezi kuwapeleka shule ikiwemo kukamtwa kwa wanao kaidi.

Hata hivyo Tanzania ni nchi ya kwanza kwa ukanda wa afrika mashariki  katika kuifanya elimu ya awali kuwa ya lazima ambapo katika sera ya elimu ya mwaka 2014 ili jumuisha elimu ya awali katika elimu ya msingi kwa kuzitaka shule zote za msingi kuwa na darasa la elimu ya awali kwa watoto wa chini ya miaka 5.

Aidha uwepo wa mazingira rafiki ya kisera kumepelekea ongezeko la uandikishaji wa watoto katika elimu ya awali kufikia 500,000 ndani ya mwaka mmoja kutoka 1,069,823 mwaka 20215 mpaka 1,562,770 mwaka 2016. Aidha kumekuwa na upungufu wa walimu wa awali ambapo wengi wao  wamekuwa wanaujuzi wa elimu ya msingi na sio elimu ya awali

 Licha ya hilo mwaka 2018 wizara ya elimu sayansi na technolojia iliripoti upungufu wa asilimia 31.7 ya walimu wa elimu ya awali wenye vigezo katika shule za serikali kutoka walimu 7,861 mwaka 2017 mpaka walimu 5,367 mwaka 2028.

 

Comments