Imani potofu ya chanjo , chazo cha watoto kupata ugonjwa wa Surua na Rubella

 

Na Baraka Lusajo – Rukwa

Imeelezwa kuwa imani potofu kwa waumini wa makanisa ya Whatch tower juu ya masuala ya chanjo imekuwa chanzo cha waumini hao kugomea watoto wao kupata chanjo mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na serikali ili kuwalinda watoto wenye umri kuanzia miezi 9 hadi 59.

Katika picha ni waumini wa kanisa la whatch tower katika kijiji cha Kalambo wakigomea zoezi la chanjo ya Surua na Rubella mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya.

Utafiti uliofanywa na Kalambodc blog umeonesha kuwa asilimia 80 ya wazazi na walezi ambao ni waumini wa makanisa ya whatch Tower wana imani potofu  juu ya mazoezi ya chanjo ambayo yamekuwa yakitolewa na serikali na hivyo kujikuta wakigomea mazoezi hayo licha ya kutambua kuwa kufanya hivyo ni kosa kisheria.

Andrea Mwakalinga ambaye ni askofu msaidizi wa makanisa ya (FPCT) mkoani Rukwa akiwa ofisini kwake, alisema elimu ya chanjo  kwa watoto bado inahitajika kwani kanisa la Whatch tower limekuwa likipinga chanjo hiyo kwa muda mrefu licha ya kujua kuwa kufanya hivyo ni kosa kwa mujibu wa sheria za Tanzania  na kusisitiza idara za afya kuwekeza zaidi katika  utoaji wa elimu.

Hata hivyo waumini wa kanisa hilo katika kijiji cha Kalambo kilichopo mpakani kati ya nchi ya Tanzania na Zambia wilayani Kalambo waligomea watoto wao wenye umri kuanzia miezi 9 hadi 59 kupata chanjo ya Surua na Rubella ambayo zoezi lake lilianza kufanyika tarehe 15/2/2024 na kusababisha watoto 9 kutoka kwenye familia  za watu wanaoabudu kwenye kanisa hilo kutokupata chanjo hiyo.

Kiongozi wa kanisa hilo Pascal Joseph, alisema wamegomea watoto wao kupata chanjo hiyo kutokana na zoezi hilo kuwa kinyume na maadili ya kanisa lao na kubainisha kuwa tangu kuanzishwa kwa kanisa hilo wamekuwa wakigomea mazoezi yote ya chanjo ikiwemo chanjo ya polio na chanjo zingine.

Katika picha ni mkuu wa wilaya ya Kalambo Lazaro Komba akiwa ofisini kwake 

Mkuu wa wilaya ya Kalambo Lazaro Komba,ambaye licha ya kukiri  waumini hao kugomea watoto wao kupata chanjo hiyo,alisema watu saba katika kijiji cha Kalambo walikamatwa na kufikishwa mahakamani kwa hatua zaidi za kisheria na kwamba walikamatwa wakikabiliwa na kosa la kuwazuia wataalamu wa afya kufanya kazi yao sambasamba na kuwanyima watoto wao haki ya kupata chanjo.

Aliongeza kwa kusema kuwa watoto wote ambao walishindwa kupatiwa chanjo kutokana na upinzani kutoka kwa wazazi wao, wamewekewa utaratibu maalumu utakaowawezesha kupata chanjo na kusema zoezi hilo ni la kitaifa na lengo la serikali ni kuhakikisha watoto wote wenye umri kuanzia miezi 9 hadi miezi 59 wanapata chanjo.

Alisema kila mwaka changamoto ya waumini wa makanisa hayo kugomea mazoezi ya chanjo yamekuwa yakijitokeza ambapo kwa mwaka huu changamoto hiyo ilijitokeza zaidi katika vijiji vya Kaluko, Kalambo na  Kasanga na kwamba tatizo lilianzia kwenye chanjo ya polio ambayo ilikuwa ikihusisha watoto wenye umri wenye umri wa miezi 9 hadi 59.

Kwa upande wake mganga mkuu wa wilaya hiyo DKT  Emanuel Mhanda  akiwa ofisini kwake, alisema kuanzia mwezi Januari 2023 hadi kufikia mwezi  februari 2023 watoto 250 waligundulika kuwa na ugonjwa wa Surua na Rubella na kwamba ugonjwa huo ulianzia katiika vijiji vya Tunyi, Ilonga na badae kuenea zaidi katika vijiji cha Msanzi ambako watoto 16 waligundulika kuwa na ugonjwa huo.

Alisema kwa kutambua umuhimu wa zoezi hilo kwa kushirikiana na wizara ya Afya walianzisha kampeni ya kutoa chanjo nyumba kwa nyumba kwa watoto kuanzia miezi 9 hadi 59 na kufanikiwa kutoa chanjo kwa watoto 45,274 sawa na asilimia 105 dhidi ya walengwa 42,805 katika vijiji 111 vya wilaya hiyo huku lengo ikiwa ni kuwakinga watoto kupata maambukizi ya ugonjwa huo  kutokana na kuenea sehemu mbalimbali.

Alisema kwa kutambua hilo wameanzisha mpango wa kutoa elimu nyumba kwa nyumba kwa wazazi na walezi sambasamba na kuyakutanisha makundi mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini  ambao watawezesha kusambaza elimu hiyo  kwa waumini wao makanisani juu ya umuhimu wa zoezi hilo.

Awali akiongea ofisini kwake kamanda wa jeshi l

    Katika picha ni kamanda wa polisi mkoani Rukwa Shrack Masija akiwa ofisini kwake.

a polisi mkoa wa Rukwa kamishina mwandamizi wa jeshi la polisi,mkoa Shadrack Masija, alisema katika kufanikisha zoezi hilo walifanikiwa kuwakamata watu saba ambao ni waumini wa kanisa la Whatch tower katika kijiji cha Kalambo kisha kuwafungulia kesi mahakamani na kuhukumiwa kutumikia kifungo cha mwaka mmoja jela baada ya kugomea zoezi la chanjo kwa watoto wao na kusema waumini hao walihukumiwa katika mahakama ya mwanzo Matai iliopo wilayani Kalambo.

Katika picha ni mkurugenzi wa shirika la Vipamaru mkoani Rukwa akizungumza na vyombo vya habari .
Hata hivyo wadau wa watoto kutoka mashirika  yasiyo kuwa ya kiserikali mkoani Rukwa akiwemo Mosses Mwangata  kutoka shirika la Vipamaru, walisema serikali haina budi kuweza kutoa elimu kwa wananchi kupitia mikutano ya hadhara sambasamba na kuyakutanisha makundi mbalimbali ya kijamii ikiwemo  viongozi wa dini ambao watasaidia kusambaza elimu kupitia makanisa yao.

Alisema serikali ya Tanzania kupitia sera ya afya ya mwaka 2017 imewekeza  katika kuboresha uhai wa mama na mtoto kupitia utoaji wa huduma za afya  bure kwa akina mama wajawazito ,na watoto chini ya miaka 5. Aidha mpango huo umeweka mazingira wezeshi ya kupunguza magonjwa na vifo vya akina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kwa kutoa huduma bora.

Hata hivyo uwekezaji wa serikali  ya Tanzania katika  uhai wa mtoto unaonekana dhahiri kwenye kupungua kwa vifo vya watoto kati ya mwaka 2010 na 2015 ambapo kiwango cha vifo vya watoto wachanga kuazia miezi 0-28 vimepungua kutoka vifo 40 hadi 25 kwa kila vizazi hai1000 huku vifo vya watoto wachanga kuanzia miezi 0-28 vikipungua kutoka vifo 99 hadi 43 kwa kila vizazi hai.

Comments