Akina mama wajawazito kujifungulia nchi jirani ya Zambia kutokana na zahanati kuzingilwa na maji ya ziwa Tanganyika
Wakazi wa kijiji cha Kipwa kilichopo mpakani kati ya nchi ya Tanzania na Zambia wameanza kutekeleza agizo la Serikali la kuwataka kuhamia maeneo ya miinuko ndani ya siku 90.
Kijiji
cha kipwa kinapatikana kata ya Kasanga wilaya ya Kalambo kando ya ziwa
Tanganyika, kutokana na jiografia hiyo kimekuwa kikikabiriwa na ongezeko la
maji ya ziwa Tanganyika.
Hata hivyo mwanzoni mwa mwaka 2021 kijiji hicho kilikumbwa na mafuriko ya maji yaliyokuwa yamesababishwa na kufurika kwa ziwa Tanganyika na kusababisha kaya 209 kukosa makazi na huku baadhi ya wananchi wakilazimika kuishi kwa majirani na sehemu za ibada huku Taasisi za Serikali zikikumbwa na kadhia hiyo.
Licha
ya hilo mnamo tarehe 30 Aprili 2021 kamati ya wataalamu wa maafa kutoka
Halmashauri ya Kalambo ikiongozwa na kaimu mkurugenzi Ndg. Jabiri Ally ilifika
kijijini hapo kwa dhumuni la kujionea adha hiyo na kubaini asilimia 70 ya
wakazi wa kijiji hicho kupatwa na adha hiyo,
Kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Jabiri Ally, alisema nyumba nyingi zikiwemo za watumishi, zahanati na shule ya msingi nazo zimezungukwa na maji na kuathiri utoaji huduma za afya na elimu.
“pia
hali ya vyoo kwa sasa sio nzuri jambo ambalo lina hatarisha kutokea kwa janga
jingine la mlipuko wa magonjwa kama kipindupindu na uti wa mgongo’’. alisema
Jabiri
Hata hivyo kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya hiyo ikiongozwa na mwenyekiti wa kamati hiyo Mhe. Kalorius Misungwi ilitembelea kijiji hicho na kuamuru wananchi wote kuhamia maeneo ya miinuko ndani ya miezi mitatu agizo ambalo lilipokelewa kwa shangwe kubwa na wakazi wa kijiji hicho.
Kamati
hiyo pia ilitembelea maeneo ya makazi mapya ya wakazi wa kjiji hicho pamoja na
maeneo ya kujenga taasisi za Serikali ikiwemo shule na zahanati.
Awali
akiongea na wakazi wa kijiji hicho mwenyekiti wa kamati ya ulinzi na usalama ya
wilaya hiyo Mhe. Kalorius Misungwi, alisema kijiji hicho kina jumla ya kaya 357
na kaya 209 zimekosa makazi na kaya 144 ndizo zilizo salia kwa hivi sasa.
Hata hivyo miongoni mwa changamoto kubwa inayowakabiri wakazi wa kijiji hicho katika maeneo mapya ya makazi wanayotarajia kuhamia ni ukosefu wa huduma ya maji pamoja na barabara.
Ziwa
Tanganyika lina urefu wa km 673 na upana wa km72 huku eneo lote likiwa na km2
32,900 na ujazo wa km3 18,800 huku urefu wa ufukwe ikiwa ni km
1,828.
Ziwa Tanganyika limezungukwa na nchi ya
Tanzania, Congo, Burundi na Zambia huku wananchi kutoka sehemu zote za nchi
hizo wakilitegemea katika shughuli za uvuvi na usafiri.
licha
ya uwepo wa ziwa hilo lakini bado kumekuwa na changamoto ya mabadiliko ya tabia
ya nchi, ambapo kwa mwaka 2020 /2021 kumekuwa na ongezeko la kupwa na kujaa kwa
ziwa hilo hali ambayo imekuwa ikiwasababishia hasara wananchi na Serikali kwa
ujumla.
March
30 /2021 kulitokea mabadiliko ya tabia ya nchi ambapo ziwa hilo lilijaa na kufunika
kijiji na eneo lenye miundombinu muhimu ya huduma kwa umma. Miongoni mwa miondombinu
iliyokumbwa na janga hilo ni viwanda, masoko na makazi ya wananchi likiwemo
soko la samaki la Kasanga.
Comments
Post a Comment