Rais
wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, atafanya ziara ya kikazi nchini Kenya siku ya
Jumanne.
Rais
Samia atakuwa katika ziara nchini humo kwa siku mbili ambapo atapokelewa na
Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta.
Ziara
hiyo ya rais Samia ni muendelezo wa jitihada za nchi hizo mbili kuboresha na
kuendeleza uhusiano wa muda mrefu na itakuwa ndio ziara ya pili nje ya taifa
lake kwa rais Samia tangu alipochukua madaraka kutoka kwa hayati Dkt John
Magufuli .
Alifanya
safari yake ya kwanza akiwa Rais nchini Uganda mnamo Aprili 11 na Rais Yoweri
Museveni akielezea kuwa lengo la ziara yake ni kuimarisha uhusiano wa nchi
mbili na kumaliza makubaliano ya mradi wa Bomba la Mafuta Ghafi kutoka nchini
Uganda.Uganda na Tanzania zilisaini mikataba mitatu yenye nia ya kuendeleza
sekta ya mafuta na gesi ya Uganda, wakati wa ziara ya hiyo.
Akiwa nchini Kenya atafanya mazungumzo na mwenyeji
wake, Rais Uhuru Kenyatta kisha atalihutubia Bunge la Kenya litakalojumuisha
Wabunge wa Mabunge yote mawili ya nchi hiyo. Taarifa ya Ikulu nchini Tanzania
imeeleza.
Aidha, Rais Samia
atahudhuria na kuhutubia mkutano wa jukwaa la wafanyabiashara wa Kenya na
Tanzania utakaofanyika jijini Nairobi kwa lengo la kujadiliana masuala yahusuyo
fursa za kibiashara na uwekezaji zilizopo nchini Tanzania na Kenya kwa mujibu
wa taarifa iliyotumw ana kurugunzi ya mawasiliano ya Ikulu
Rais Samia amedhihirisha
si mara moja kuhusu nia yake ya kuvutia wawekezaji kwenda Tanzania . Ziara hii
yake nchini Kenya itakuwa mojawao ya jitihada za kuwahakikishia mazingira bora
wawekezaji walioko nchini Kenya kufungua biashara zao nchini humo.
Kulikuwepo awali na
changamoto kwa wawekezaji hasa kutoka mataifa ya kigeni kuendeleza shughuli zao
za kibiashara nchini Tanzania na hilo rais Samia alilitaja hata katika hotuba
yake kwa bunge la Tanzania alipoeleza umuhimu wa serikalia kuhakikisha kwamba
wawekezaji wanapata urahisi wa kuendesha shughuli zao nchini mwake
Comments
Post a Comment