Hospitali ya wilaya ya kalambo mkoani Rukwa kwa kipindi cha miezi sita imewezesha wanawake 860 kujifungua kati yao wanawake 741wakijifungua kwa njia ya kawaida na 119 wakijifungua kwa njia ya upasuaji huku vifo vya mama na mtoto vikipungua kutoka 11-8 kwa mwaka 2023.
Hayo
yamebainishwa na mratibu wa huduma za mama na mtoto wilayani humo Bakari
Ndarusi wakati wa utoaji elimu ya kwa wanawake wanao jifungua katika hosptali
hiyo,ambapo amesema licha ya hilo hospitali hiyo inahudumia wastani wa watoto 180 hadi 200 na watoto njiti 6 kwa
kila mwezi.
Aidha amesema hosptali hiyo inahudumia wanawake wanaojifungua wapatao 8-9 kwa siku na kubainisha kuwa hadi kufikia mach 2024 wanawake 2218 wamepatiwa huduma za mama na mtoto na kwamba kila mwezi wanawake 164 wamekuwa wakihudhuria huduma hizo .
Kwa
upande muuguzi mkuu wa hosptali hiyo , Diana Didi amesema licha ya hilo hospitali
hiyo imekuwa ikihudumia wanawake 30 kwa siku na kuwataka wanawake kujenga
mazoea ya kuwahi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya pindi wanapopatwa na uchungu wa kujifungua
ili kuokoa
vifo vya mama na mtoto.
Kwa
upande wake Kaimu mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Sunday Wambula akiwa
ofisni kwake amebainisha kuwa licha ya hilo halmshauri imepokea fedha million
mia nne kwa ajili ya umaliziaji wa zahanati 8 na shilingi million mia tatu kwa
ajili ya ununuzi wa vifaa tiba vituo vipya vya afya.
Comments
Post a Comment