JAMII YATAKIWA KUWAHUSISHA WATOTO KATIKA UTUNZAJI WA MAZINGIRA

 Na. Zillipa Joseph, Katavi



Katibu Tawala wa wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi Geofrey Mwashitete ameitaka jamii kujenga mazoea ya kuwahusisha watoto katika shughuli mbalimbali za maendeleo ikiwemo utunzaji wa mazingira hali itakayopelekea manufaa makubwa kwa nchi kwa nyakati za sasa na zijazo

Mwashitete ametoa kauli hiyo katika kilele cha wiki ya mazingira wilaya iliyofanyika katika shule ya msingi Kapemba kata ya Mishamo wilayani humo

Alisema sehemu mojawapo ya kufikisha ujumbe kwa jamii nzima ni kuhusisha watoto hasa wenye umri mdogo kwani wao wanashika sana wanachoambiwa

“Hawa watoto ukiwaambia wanabeba hivyo hivyo lilivyo, sio watu wazima wana mambo kibao kichwani, kwa hiyo hawa watoto wakihusishwa ipasavyo hakika kutakuwa na mabadiliko chanya siku zijazo’ alisema Mwashitete

Mwashitete amekabidhi miche 3,000 ya miti ya matunda kwa watoto hao ili ikapandwe katika mazingira wanayoishi


Comments

Post a Comment