Jumla ya wanafunzi 7563 wa madarasa ya awali wilayani Kalambo mkoani Rukwa kati yao wavulana wakiwa 3687 na wasichana 3906 wameripoti shule na wanafunzi 9765 kati yao wavulana wakiwa 4830 na wasichana 4935 wa darasa la kwanza wameripoti shule na kuendelea na masomo.
Hata hivyo kupitia ripoti iliotolewa na
mkuu wa wilaya ya Kalambo kwenye vyombo vya habari Januari 14/2024 imeeleza kuwa
Jumla ya wanafunzi 6389 waliandikishwa na kujiunga na elimu ya awali kati yao
wavulana walikuwa 3125 na wasichana 3289.
Aidha kwa upande wa
shule za sekondari jumla ya wanafunzi 4,887 walichaguliwa kujiunga na elimu ya
sekondari kati yao wavulana wakiwa 2,319 na wasichana 2,568.
Comments
Post a Comment