Wakazi Vijiji Vya King’ombe Na Kansapa Waondokana Na Tatizo La Umeme


wakazi wa vijiji vya Kansapa na king’ombe wialaya ya Nkasi mkoani Rukwa wameondokana na matumizi ya mishumaa na vibatari kutokana na serikali kuwakamilishia mradi mkubwa wa umeme unao tajwa kuwawezesha kupunguza gharama za matumizi ya mafuta wakati wa uendeshaji viwanda vidogo vidogo.

Wameyasema hayo kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika wilayani humo,ambapo wamesema awali walikuwa wakilazimika kutumia vibatari na mishumaa na kwamba tangu  kufikiwa na huduma hiyo kuwafikia wamefanikiwa kuanzisha viwanda vidogo ikiwemo mashine za kusaga na kukoboa na kujikwamua kiuchumi.

licha ya hilo wameiomba serikali kutafuta ufumbuzi wa kudumu utakao saidia kuondoa changamoto ya kukatika kwa umeme.

Mapema akiongea na wakazi wa vijiji hivyo mkuu wa wilaya ya Nkasi Peter Lijualikali amesema licha ya hilo serikali imetoa fedha million 500 ili kujenga zahanati kutokana na vijiji hivyo kuwa na ukosefu wa huduma ya afya tangu kuanzishwa kwake.

Comments