Na Baraka Lusajo - Rukwa.
Mkuu
wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Lazaro Komba ameliagiza Jeshi la polisi
wilayani humo kuwakamata wazazi na walezi waliomwozesha mwanafunzi wa darasa la
saba katika shule ya msingi Mbuza kata ya Mkowe mwenye umri wa miaka 17 na kumuozesha
kwa Asulwa Sikombe mkazi wa kijiji cha Mbuza.
Taarifa
kutoka kwa kwenye uongozi wa kijiji hicho akiwemo mwenyekiti wa kijiji hicho
Alisen Machenchelwa na mkuu wa shule hiyo Fedelisi Mbuluko zimeeleza kuwa
mwanafunzi huyo Mach 2023 alitoroka kwenye makazi ya wazazi wake na kutokomea
kusiko fahamika na kwamba baada ya kurejea June 2023 wazazi wake walimua
kumuozesha kwa ndugu Asulwa Sikombe mkazi wa kijiji cha Mbuza.
Walieleza
kuwa baada ya kupata taarifa hizo waliamua kuwakamata wazazi wa binti huyo na
kuwafikisha kwenye kituo cha polisi Matai kwa hatua zaidi.
Hata
hivyo mapema akiongea ofisini kwake mkuu wa wilaya hiyo Lazaro Komba amesema
mpaka sasa Jeshi la polisi linamsaka aliyeozeshwa mwanafunzi huyo na kwamba
wazazi wawili wa mwanafunzi huyo wamekamatwa.
Licha
ya hilo alitoa wito kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kuwaozesha wanafunzi
kwani ni kosa kisheria.
Comments
Post a Comment