Mahakama ya wilaya ya Kalambo
mkoani Rukwa kwa mwaka 2022 imefanikiwa kusajiri mashauri 216 na kumaliza
mashauri 184 huku mashauri 32
yakishindwa kumalizwa kutokana na changamoto mbalimbali
Hakimu mfawidhi mkazi wa Mahakam ya wilaya ya kalambo kupitia kilele cha madhimisho ya siku ya
sheria, Nikson Tem, amesema kwa mwaka
jana Mahakama zilifanikiwa kusajiri mashauri 375 na kumaliza mashauri
367 na kubakiza mashauri 8 na kwamba idadi hiyo ni pamoja na Mahakama za mwanzo
‘’maadhimisho ya siku ya sheria
nchini huambatana na kauli mbiu au maudhui na kwamaka huu kauli mbiu yeu ni
umuhimu wa utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi katika kukuza uchumi
endelevu ;wajibu wa mahakama na
wadau’’ alisema Tem
Alisema kauli mbiu hiyo imebeba
ujumbe mahususi kuhusu wajibu wa mahakama na wadau wake katika kutumia njia ya
usuruhishi katika kutatua migogoro kwa lengo la kukuza uchumi endelevu
Mapema kiongea kupitia maadhimisho
hayo wakili wa serikali Marietha Maguta , aliwakikishia wananchi na wadau wa sheria kuwa ofisi ya mwanasheria
mkuu wa serikali itaendelea
kusimamia kwa karibu maelekezo yaliotolewa na kutoa kipaumbele chs kumaliza
migogoro kwa njia ya maridhiano
‘’msisitizo wa ut
atuzi wa migogoro kwa njia ya mbadara na uikilizwaji wa mashauri kwa njia ya za kimahakama kama ulivyowekewa msingi imara kwenye sheria zetu unahitaji kuwekwa mazingira rafiki ,jambo ambalo pia limekuwa likihimizwa sehemu mbalimbali duniani’’ alisema Malietha
Kwa upande wake Deogratus Sanga ,
alisema TLC imejiwekea mkakati wa
kuanzisha kituo cha cha kimataifa cha usuluhishi wa migogoro kwa kushirikina na
wizara ya katiba na sheria ambacho kitaiweka Tanzania katika ramani ya Afrika
na dunia kwa kutekeleza dhana ya kutatua migogoro ya kibiashara za kimataifa
nay a wawekezaji kwa njia ya suluhu
Hata hivyo, Tanzania ni muhimili
ulioanzshwa na katiba ya Jamhuri ya mungano wa Tanzania ya mwaka 1977 ambayo
inatoa mamlaka kwa mahakama kuwa chombo cha kutoa haki kwa wakati na kwa
wananachi wote
Comments
Post a Comment