Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Tano Mwela Januari 22/2023 wakati wa uzinduzi wa maadhimisho ya wiki ya sheria ambayo kwa ngazi ya wilaya yamefanyika kwa kufanya matembezi kutoka eneo la Santamaria hadi katika ofisi za Mahakama ya wilaya hiyo
Amesema utatuzi wa migogoro kwa
njia ya usuluhishi ni takwa la katiba ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania ,ambapo
utekelezaji wake ni muhimu ili kuendana na kasi
ya shughuli za ukuaji wa uchumi wa wananchi
‘’hivyo njia mbadala ya utatuzi
wa migogoro inajumuisha utaratibu wa usuluhishi ,upatanishi,kurudisha mahusiano
ya kirafiki na mazungumzo kufikia makubaliano ‘’ alisema Mwela
Alisema licha ya hilo mahakama inawajibu wa kuongoza waadawa katika kufikia makubaliano ,kuandaa wataalamu
wa usuluhishi ikiwemo majaji na mahakimu kwa kuwaongezea ujuzi kwa njia ya
mafunzo ,pamoja na kuweka mazingira rafiki ya usuluhishi na kutoa elimu kwa
umma
Mapema akiongea na hadhara ya wananchi katuka maeneo
hayo hakimu mfawidhi mkazi wa mahakama
ya wilaya ya Kalambo, Nikison Tem , amesema
utatuzi wa migogoro kwa njia ya usuluhishi una faida nyingi ikiwemo upatikanaji haki kwa wakati na kwa gharama
nafuu
Hata hivyo maadhimisho ya
uzinduzi wa wiki ya sheria unafanyika
katika maeneo mbalimbali ambapo kwa ngazi ya kanda umefanyika katika mahakama kuu
kanda ya sumbawanga mkoani Rukwa na
kuzinduliwa na jaji mkuu kanda ya Sumbawanga Dastan Ndunguru,
Comments
Post a Comment