Waziri Mkuu Kassim Majaliwa ameanza ziara ya kikazi katika Mkoa wa Rukwa ambapo ametembelea na kukagua maendeleo ya ujenzi wa shule ya Sekondari ya Paramawe na hospitali ya Wilaya iliyopo Wilayani ya Nkasi.
Akiwa
katika Shule ya Sekondari Paramawe leo (Desemba 14,2022) inayojengwa kupitia
mradi wa SEQUIP ambapo ameweka jiwe la msingi la mradi huo uliogharimu Shilingi
Milioni 470 kujenga vyumba nane vya madarasa,maabara,maktaba na matundu ya
vyoo.
Akizungumza
baada ya kukagua ujenzi huo, Waziri Mkuu amemuagiza Katibu Tawala wa Mkoa huo
Rashid Mchatta kumsimamia Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi William
Mwakalambile ili ahakikishe anakamilisha maeneo ya ujenzi wa shule hiyo kwa
kutumia mapato ya ndani.
“Milioni 470 zimetumika na mmetumia zingine za halmashauri lakini miundombinu bado. Nataka shule hii ikamilike na Januari 2023 wanafunzi waingie” Alisema Majaliwa
Kuhusu
ujenzi wa hospitali ya Wilaya Nkasi, Waziri Mkuu aliewaeleza wananchi kuwa
serikali itaendelea kukamilisha miradi yote ya afya ikiwemo kuhahikisha vifaa
tiba vinapatikana kwa ajili ya wananchi kupata huduma.
Aidha,
Waziri Mkuu amemwagiza Naibu Katibu Mkuu
Tamisemi -Afya kukutana na uongozi wa halmashauri ya Nkasi ili kujua
kwanini mradi ya ujenzi wa majengo saba ya hospitali ya wilaya haujaanza wakati
tayari fedha zilikwishatolewa na serikali.
“Naibu
Katibu Mkuu Tamisemi urudi hapa Nkasi kesho kufuatilia kwanini majengo saba
hayajaanza wakati fedha ipo” aliagiza Waziri Mkuu Majaliwa.
Katika
hatua nyingine Majaliwa ameagiza Mkuu wa Mkoa huo na Katibu Tawala wa Mkoa
kuitisha kikao cha mawakala wa mbolea mapema iwezekanavyo ili kuhakikisha
wakulima wanapata pemebejeo hiyo muhimu kwa kuwa serikali imekwisha toa fedha
za ruzuku .
Kwa upande
wake Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Queen Sendiga alisema mkoa unaendelea na usimamizi
wa shughuli za maendeleo na kuwa wananchi watapata huduma stahiki.
Waziri Mkuu
kesho ataendelea na ziara yake kwenye wilaya za Kalambo na Sumbawanga.
Comments
Post a Comment