Dc Kalambo Asisisitiza Wananchi Kulinda Miundombinu Ya Maji


Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Tano Mwela amewataka wananchi wilayani humo kujenga mazoea ya kutunza miundombinu ya maji ili iweze kudumu na kuwa endelevu kutokana na serikali kutumia fedha nyingi katika kuiboresha na kuijenga


Aliyasema hayo wakati wa ziara ya kamati ya usalama  ya wilaya hiyo wakati wa ukaguzi wa mradi wa maji katika kijiji cha Mpombwe unaotekelezwa na wataalamu wa ndani (Force Account ) kwa gharama ya shilingi milion 304,729,750.00  na  kusema mradi huo umejengwa kupitia ufadhili wa fedha za Benk ya Dunia kupitia program ya PforR na kwamba utahudumia wakazi wapatao 3,058 na kudumu kwa miaka 20.

Aidha aliwataka wananchi kuwa walinzi  kwa kutoa taarifa kwenye mamlaka husika dhidi ya mtu au watu wanaoharibu miundombinu ya maji ili waweze kuchukuliwa hatua za kisheria

Mapema akiongea kupitia ziara hiyo Kaimu meneja wa Ruwasa wilayani humo Francis Mapunda , alisema katika kuhakikisha mradi huo unakuwa endelevu kimeundwa chombo cha watoa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSO) kijulikanacho  kwa jina la KAPOMBWE ambacho kitasimamia shughuli za uendeshaji na matengenezo ya miradi ya vijiji vya kata ya Kisumba na Mpombwe


Baadhi ya wananachi kijiji hapo waliipongeza serikali kwa kukamilisha mradi huo na kwamba utawawezesha kuondokana na adha ya kutembea umbali mrefu wakati wa kutafuta huduma ya maji maeneo ya mbali

Comments