Na Baraka Lusajo – Rukwa
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa
Queen Sendiga ameelekeza halmashauri zote mkoani humo kuandaa maadhimisho ya
wiki ya utoaji elimu ya lishe bora katika ngazi za vijiji ili kukabiliana na
tatizo la udumavu.
Ametoa kauli hiyo mjini Sumbawanga wakati wa hafla ya kukabidhi
pikipiki Kumi na Mbili (12) kwa maafisa lishe wa halmashauri zilizotolewa na
serikali kwa ajili ya kukabiliana na tatizo la udumavu ambao kwa Rukwa upo
asilimia 47.9 kwa takwimu za mwaka 2018.
Sendiga alibainisha kuwa
maadhimisho hayo yakifanyika itakuwa jukwaa zuri la wataalam wa lishe kutoa
elimu ya uandaaji vyakula bora na ulaji sahihi kwa kutumia vyakula
vinavyopatikana kwenye mazingira ya Rukwa kwa kuwa mkoa huo ni mzalishaji
mkubwa wa mazao ya chakula na kuifikia jamii kwa wakati ili watoto waweze
kupata lishe bora
Akitoa taarifa ya vifaa
hivyo, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Ibrahim Isaack alisema jumla ya
pikipiki Kumi na Mbili zimetolewa kwa Halmashauri za Kalambo (4), Sumbawanga
Vijijini (3), Nkasi (3) na Manispaa ya Sumbawanga (2).
Dkt. Ibrahim alisema
pikipiki hizo zitakwenda kufanya kazi ya elimu ya lishe, kuboresha utoaji
chanjo kwa watoto wenye umri chini ya
miaka 5 na kufuatilia magonjwa ya milipuko vijijini.
Mwisho.
Comments
Post a Comment