Halmashauri Ya Kalambo Yazindua Rasmi Tamasha La Ngoma Za Asili

 


Na IO – Kalambo.

Halmashauri ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa imeanzisha kampeni ya kusaka vipaji vya vijana kupitia Sanaa na utamaduni kwa kupita mtaa kwa mtaa ili kuzindua matamasha ya ngoma za asili kwa lengo la kupata vikundi ambayo vitashindanishwa katika mashindano ya wilaya.

Mapema akiongea kupitia uzinduzi wa tamasha la ngoma za asili lililofanyika katika kijiji cha mkowe wilayani humo afisa utamaduni wilayani humo Evance Showo amesema Tamasha la LINGOMA FESTIVAL 2022 limeasisiwa na Ofisi ya Utamaduni na kuhusisha vikundi vinne(4) vya ngoma za Asili vilivyopo katika kijiji cha Mkowe kwa malengo ya kuunga Mkono Juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan Katika kuboresha Sanaa na Utamaduni Katika nchi yetu.

Alisema licha ya hilo Tamasha limebeba Ujumbe wa “UTAMADUNI WETU FAHARI YETU” na limelenga kutoa burudani kwa jamii na kujenga Mahusiano ya vikundi vya Sanaa na Utamaduni Vilivyopo Katika Jamii.


Awali wakiongea kupitia uzindunzi huo wananchi katika maeneo hayo ambao licha ya kuipongeza serikali kwa kuanzisha Tamasha hilo wakaitaka kuweka utaratibu maalumu ambao utasaidia vikundi hivyo kutambuliwa ili viwe na uwezo wa kukopesheka kupitia taasisi  za kifedha.

Comments