Na IO –Kalambo
Halmashauri
ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa imefanikiwa kuhesabu watu 65,846 sawa na
asilimia 99.93 kati ya watu 65 ,894 ambao walikisiwa kuhesabiwa tangu kuanza
kwa zoezi la sensa na makazi Agosti 23/2022 huku wananchi waliopata fursa ya
kuhesabiwa kwenye zoezi hilo wakiipongeza serikali kwa kuweka mazingira rafiki na
wezeshi yaliyowezesha kuhesabiwa kwa haraka na kuendelea na shughuli zingine za
ujenzi wa taifa.
Zoezi la sensa na makazi Lilianza kufanyika rasmi kitaifa Agosti 23/2022 ambapo kwa wilaya ya Kalambo zoezi hilo lilianzia katika makazi ya mkuu wa wilaya hiyo Tano Mwela ambaye mnamo majira ya saa sita usiku na dak 1 alihesabiwa kama raia namba moja wa wilaya hiyo na kufuatiwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmshauri hiyo Shafi Mpenda.
Hata
hivyo tangu kuanza kwa zoezi hilo wananchi walionyesha mwitiko mkubwa kwa
kujitokeza kuhesabiwa na kutoa ushirikiano kwa makarani wa zoezi hilo hatua iliyopelekea
kumalizika haraka kwa zoezi hilo.
Awali akiongea baada ya kamati ya usalama ya wilaya hiyo kutembelea na kukagua maendeleo ya zoezi la sensa na makazi katika maeneo tofauti ya wilaya hiyo, Mkuu wa wilaya hiyo Tano Mwela , alisema zoezi hilo limekwenda vizuri na kufanikiwa kufikia malengo ya serikali.
‘’Wilaya
yetu ya Kalambo tulikuwa na maoteo ya kuhesabu watu 65,894 na mpaka sasa
tumefanikiwa kuhesabu watu 65,846 sawa na asilimia 99.93 kwa hiyo tumefanikiwa
kuhesabu watu wote kwa wilaya ya kalambo na kama kuna waliobakia basi ni
wachache sana ambao tunaendelea kuwamalizia.’’Alisema Mwela.’’
Licha
ya hilo alilisitiza wananchi kutoa ushirikiano wakati wa dodoso la majengo
ambalo linatarajiwa kuanza kufanyika Rasmi Agosti 30/2022.
Comments
Post a Comment