Wananchi Katika Kijiji Cha Singiwe Waazimia Kuchukua Hatua Dhidi Ya Wazazi Walioshindwa Kutoa Malezi Kwa Watoto Wao.
Na Baraka Lusajo- Rukwa
Wananchi
katika Kijiji cha Singiwe kata ya Lyowa wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameazimia
kuchukua hatua kali dhidi ya wazazi na walezi ambao watabainika kushindwa kudhibiti
uzurulaji wa watoto wao nyakati za usiku.
Hatua hiyo inakuja baada ya kujitokeza wimbi la watoto kuanzia miaka 3-8 kukutwa mitaani nyakati za usiku wakizurula na wengine kukutwa kwenye kumbi za kuoneshea video huku wazazi wao wakionekana kutokuwa na habari na familia zao.
Akiongea kupitia mkutano wa hadhara
uliofanyika kijijini hapo,Mwenyekiti wa kijiji cha Singiwe Donard Songolo , alisema kwa kutambua umuhimu
wa ulinzi wa watoto wameanza kuchukua hatua dhidi ya wazazi ambao wamekuwa
wakishindwa kuwadhibiti watoto wao nyakati za usiku na kuishia kuangalia video
kwenye mabanda umiza huku wengine wakilazimika kulala kwa majirani kutokana na
ukosefu wa uangalizi.
‘’tunataka
wazazi wawe waangalizi na walinzi wa watoto wao hivyo mzazi au mlezi ambae
ataonekana kushindwa kumlea mtoto wake atachukuliwa hatua kali za kisheria
kwani tumeshuhudia kila siku watoto
hususani kuanzia miaka 3 wanakuwa kwenye sehemu za kuoneshea video muda
ambao walipaswa kuwa nyumbani hali ambayo ni hatari. Alisema chongolo
Diwani
wa vitimaalmu katika tarafa ya,Matai wilayani humo Yuster Kajema , alisema lengo la serikali ni
kuhakikisha watoto wote wanalindwa ikiwemo kutambua haki zao za msingi ,
kupatiwa elimu , malazi na mavazi na kwamba kwa kufanya hivyo ndivyo itaonekana
kweli tunawalinda.
‘’lengo
la serikali ni kuhahakikisha huduma za malezi jumuishi ya watoto zinawafikia
watoto wote wenye umri kuanzia miaka (0-8) pamoja na kuzingatia masuala ya
jinsia, watoto walio katika mazingira hatarishi kwa mfano watoto wote wenye VVU,
Yatima ,watoto wanao umwa sana pamoja na wenye utapia-mlo ,watoto walipo mahabusu
,kambini na wenye changamoto katika ukuaji
wote kwa umoja wao wanapaswa kulindwa na kupata stahiki muhimu.’’alisema
Kajema.
Hata
hivyo katika kuhakikisha haki za watoto zinatambulika na kutekelezwa, Tanzania
ni miongoni mwa nchi zilizoridhia na kusaini mkataba wa kimataifa wa haki za
mtoto na mapendekezo ya kamati Na. 7 ya mwaka 2005 katika kutekeleza haki za
watoto.
Comments
Post a Comment