Mwandishi Wa Kituo Cha ITV Na Radio One Mkoani Rukwa Apata Hati Ya Pongezi Kwa Kuandika Habari Za Michezo Ya Watoto Chini Ya Miaka 8 Kwa Kipind Cha Miaka 2 Mfululizo.


Mwandishi wa habari wa kituo cha ITV na Radio one mkoani Rukwa Baraka Lusajo kwa mara nyingine amepata hati ya pongezi pamoja na zawadi kutoka kwa walimu wa michezo na maafisa michezo kutoka mikoa ya Rukwa Katavi na Songwe baada ya kuonesha uzalendo wa hali ya juu na kujitoa kwa moyo wake wote katika kazi yake ya uandishi wa habari akiandika habari mbalimbali za kijamii ikiwemo kukuza vipaji vya watoto wa shule za msingi kuanzia ngazi ya awali.

Mwandishi huyo amepatiwa hati hiyo kutokana na kuandika habari za watoto katika kipengele cha michezo na zilizo wezesha kuongeza ali ya ujifunzaji darasani.

Kaimu afisa michezo mkoani Rukwa Amos Mmewa, alibainisha kuwa uwepo wa michezo kwa watoto imekuwa ikisadia kuongeza ali ya uelewa darasani kwa watoto na kwamba mpaka sasa wameweka mkakati wa kutoa elimu kwa waalimu wa michezo kutoka mikoa mitatu ikiwemo Rukwa, Katavi na Songwe lengo likiwa ni kuhakikisha watoto wa awali wanapewa kipaumbele katika michezo.

‘’walimu hawa wa michezo wanaenda kuwa msaada mashuleni katika kuendeleza vipaji vya watoto kwa kubuni michezo mbalimbali ambayo inaenda kusaidia katika swala la makuzi na maendeleo ya watoto kiakili’’ alisema mmewa.

Kwa upande wake mkufunzi kutoka chuo cha michezo cha Malya Erick Mfugale, alisema michezo hiyo inalenga watoto wenye umri kuanzia  miaka 3  na kwamba lengo likiwa ni kuongeza kiwango cha ulewa darasani.

Alisema Tanzania ni nchi ya kwanza katika ukanda wa Afrika Mashariki katika kutoa elimu ya awali na kuifanya kuwa ya lazima kwenye sera ya elimu na mafunzo ya ufundi na kwamba kwa kutambua hilo wadau wa michezo wameona kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa maafisa michezo na walimu wa michezo ili kuwajengea uwezo zaidi juu ya umuhimu wa michezo kwa wanafunzi wa awali.

‘’vilevile mtaala wa elimu ya awali unasaidia ujifunzaji kupitia michezo na mwongozo wa serikali wa mwaka 2016 wa elimu bila malipo hujumuisha elimu ya awali .Aidha uandikishwaji wa elimu ya awali  ni kiashiria muhimu kilicho ingizwa  katika mpango wa kitaifa wa maendeleo ya miaka  mitano 2016/17-2020/21.

 

 

Comments