Watakao Vurunda Zoezi La Chanjo Ya Polio Kukiona Cha Mtema Kuni ‘’ Dc Kalambo’’


Mkuu wa wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa Tano Mwela amemuagiza mganga mkuu wa wilaya hiyo kuhakikisha zoezi la utoaji chanjo ya polio kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano linafanyika kwa weredi na kwa ustadi mkubwa na kusisitiza kuchukua hatua kali za kisheria dhidi ya watumishi ambao watabainika kuandika data za uongo wakati wa uendeshwaji wa zoezi hilo.

Ugonjwa wa polio ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya polio ambapo kwa mara ya mwisho Tanzania ilipata mgonjwa wa polio Julai 1996 na kuja kugundulika tena Februal 2022 katika nchi jirani ya Malawi ambako mgonjwa wa kwanza alipatikana katika mji mkuu wa Malawi.

Hata hivyo tathimini iliyofanywa na wizara Afya kwa ushirikiano na shirika la afya Duniani {WHO} nchi ya Tanzania ilionekana kuwa miongoni mwa nchi zilizo katika hatari kubwa ya kupata maambukizi ya ugonjwa wa polio endapo kama hatua madhubuti hazitochukuliwa kwa haraka.


Awali akiongea wakati wa kikao ch a mafunzo kwa kamati ya msingi ya Afya ngazi ya jamii {PHC} Mganga mkuu wilayani humo Dkt Eugen Lutaisire,alisema zoezi hilo litafanyika nyumba kwa nyumba na mtoto kwa mtoto.

‘’Sambamba na uchanjaji huduma zingine zitatolewa ikiwemo elimu ya chanjo,kuimarisha huduma za chanjo katika vituo vya kutolea chanjo  ikiwemo kuwatafuta na kuwafuatilia watoto wote wenye umri  chini ya miaka  miatano 5, ambao wamepata  ulemavu wa ghafla  tepetepe {washukiwa wa ugonjwa wa polio} na kutoa taarifa katika vituo vilivyopo karibu kwa uchunguzi na kubaini ugonjwa huu wa polio’’ alisema DkT Eugen.

Alisema ugonjwa wa Polio unasababishwa na Virusi vya polio na husababisha kupooza na hatimaye kifo na kusisitiza kuwa virusi vya polio huingia mwilini kwa njia ya mdomo , kwa kunywa maji au chakula ambacho kimechafuliwa na kinyesi.

Awali akifungua kikao cha PHC wilayani humo mkuu wa wilaya ya Kalambo Tano Mwela,alisema hata sita kuchukua hatua dhidi ya watumishi ambao watabainika  kutoa data za uongo wakati wa uendeshwaji wa zoezi hilo  na kusisitiza taarifa zote kuwekwa kwa maandishi na kwa kufuata utaratibu.

‘’Taarifa zote ziwe kwa maandishi na zoezi hili nitafuatilia kwa ukaribu hivyo nataka zoezi hili lifanyike kwa weredi mkubwa’Alisistiza Mwela.

Comments