Halmashauri ya wilaya ya Kalambo
mkoani Rukwa imeazimisha miaka 58 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar kwa
kufanya usafi kuzunguka maeneo ya hospitali ya wilaya hiyo huku wananchi wilayani
humo wakihimizwa kulifanya zoezi hilo kuwa endevu kwa kufanya usafi kila siku
badala ya kusubiri matukio ya kitaifa kwa lengo la kufanya mazingira kuwa safi
muda na wakati wote.
Wakiongea wakati wa shughuli za usafi wa mazingira kuzunguka maeneo ya hospitali ya wilaya hiyo kama sehemu ya kuazimisha miaka 58 ya muungano, viongozi wa serikali wilayani humo wamesema zoezi hilo linapaswa kuwa endelevu.
Akiongea wakati wa shughuli za usafi wa mazingira, mkuu wa wilaya hiyo Tano Mwela, alisema wameazimisha miaka 58 ya muungano wa Tanganyika kwa kufanya usafi kuzunguka hospitali ya wilaya hiyo kama njia ya kuhamasisha jamii kujenga mazoea ya kufanya usafi kila siku na kuwataka wananchi kujenga mazoea ya kufanya usafi kila wakati pindi wanapopata nafasi ili kuyafanya mazingira kuwa bora na salama.
Mkurugenzi
mtendaji wa Halmashauri hiyo Shafi Mpenda,alisema swala la usafi ni maelekezo
ya serikali ambayo yanawataka wananchi
na watumishi wa umma kufanya usafi kila mwezi kuzunguka maeneo yao husika na kwamba wameazimisha
miaka 58 kwa kufanya usafi katika maeneo hayo kama njia ya kuunga mkono jitihada
za serikali juu ya uwekezaji wa hospitali
hiyo.
‘’Kikubwa sisi kama watumishi wa umma tunachokifanya ni kuwakumbusha wananchi kwamba kila mwezi lazima tufanye usafi hivyo kikubwa wananchi lazima elimu hii iwaingie ili kujua kuwa usafi ni jukumu la kila mmoja.’’ alisema Mpenda.
Hata hivyo Halmashauri
mbalimbali mkoani Rukwa zimeazimisha miaka 58 ya muungano kwa kufanya shughuli
tofauti, ambapo watumishi kupitia ofisi ya mkuu wa mkoa wa Rukwa imeazimisha miaka
58 kwa kufanya usafi wa mzingira kuzunguka maeneo yote ya ofisi ya mkuu wa mkoa
wa Rukwa.
Mkirikiti ameshiriki zoezi
hilo la usafi (26.04.2022) katika maeneo ya Ofisi yake zilizopo mjini
Sumbawanga huku akisisitiza watanzania
kueendelea kuwa wamoja na wenye kuheshimiana hatua inayokuza utaifa.
“Leo ni siku muhimu kuona
kama watumishi tukiwa na umoja na upendo kati yetu wa Bara na wenzetu wa
Zanzibar kufuatia uwepo wa Muungano wa nchi zetu mbili. Tuuenzi Muungano wetu
huu ili udumu kwa vizazi vingi zaidi vijavyo” alisisitiza Mkirikiti.
Kwa upande wake Kaimu Katibu
Tawala Mkoa wa Rukwa Donald Nssoko aliwapongeza watumishi wa umma waliopo makao
makuu pamoja na taasisi zilizopo kwenye jengo la mkoa kwa kujitokeza
kuadhimisha sherehe za Miaka 58 ya Muungano kwa kufanya Usafi hatua inayoongoza
ushirikiano miongoni mwa watumishi hao.
Nae Dkt. Uwezo Kinahi
akizungumzia kwa niaba ya watumishi alieleza kuwa tukio hilo alisema
anawapongeza watanzania kwa kudumisha Muungano na kuwa kitendo cha kufanya
usafi siku ya leo ni mwendelezo wa kuonesha umoja wa watanzania mahala pa kazi.
Dkt. Kinahi amewasihi
wananchi wa Rukwa kuendeleza mshikamano wa kidugu na wananchi wa Zanzibar ili
kwa pamoja Tanzania ipige hatua zaidi ya kimaendeleo.
Watanzania leo wanaadhimisha
sherehe za miaka 58 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Comments
Post a Comment