Na Baraka Lusajo – Rukwa.
Wanawake
wilayani Kalambo mkoani Rukwa wamesema kuna umuhimu wa serikali kuangalia namna
bora ya kudhibiti vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto
ambavyo wakati mwingine vimekuwa vikijitokeza katika jamii na kuathiri makuzi
na maendeleo ya awali ya watoto
hususani wenye umri chini ya miaka 8
Waliyabainisha hayo kupitia maadhimisho ya uzinduzi wa jukwaa la uwezeshwaji kiuchumi la wanawake yaliyofanyika katika kata ya Matai wilayani Kalambo mkoani Rukwa na kusema vitendo vya ukatili wa kijinsia wakati mwingine vimekuwa vikiwaathiri zaidi akina mama wajawazito ambao wamekuwa wakikumbana na ukatili wa aina tofauti ikiwemo vipigo na kusababisha wengine kupoteza viumbe tumbo.
Akiongea
kupitia uzinduzi wa jukwaa la uwezeshwaji kiuchumi la wanawake wilayani humo,
mwenyekiti wa jukwaa hilo Ester Msigwa, alisema wanawake wajawazito ni miongoni
mwa watu ambao wamekuwa wakikabiliwa na matukio ya ukatili ambao wakati
mwingine umekuwa ukiathiri kuhudhuria huduma za afya kama huduma za mama
mjamzito.
‘’Pia wanawake wajawazito wameripotiwa kupitia aina tofauti za unyanyasaji ambapo kati asilimia 7 mpaka 10 wametajwa kupitia ukatili wa kijinsia ukiathiri kushindwa kuhudhuria huduma za afya kama huduma ya mama mjamzito, Sambamba na kiwango kikubwa cha ukatili wa kimwili dhidi ya wanawake kimekuwa kikiripotiwa hivyo kuna umuhimu wa serikali Kushirikiana na majukwaa haya ili kusaidia katika utoaji elimu.’’ Alisema Msigwa.
Kaimu
afisa maendeleo ya jamii anayeshughulika na makundi ya wanawake,vijana na watu
wenye hali ya ulemavu Yasina Nkyabonaki, alisema kwa kutambua umuhimu wa
makundi hayo Halmashauri imetoa fedha kiasi cha shilingi million hamsini ili
kusaidia makundi hayo kujikwamua kiuchumi.
Alisema,wanawake
wakiwezeshwa watakuwa na uwezo wa kulea familia zao na kuondokana na hali ya
ukali ambao wakati mwingine umekuwa ukifanyika
pengine kutokana na manyanyaso kutoka kwenye koo au familia zao husika.
Awali
akizungumza na hadhara ya wanawake kupitia maadhimisho hayo mkuu wa wilaya hiyo
Tano Mwela, alisisistiza wananchi kujiepusha na vitendo vya ukatili kwa
kuchukua hatua na kutoa taarifa za uwepo wa matukio hayo kwenye maeneo yao
husika ili serikali iweze kuchukua hatua.
Alisema
familia zinapaswa kuwekeza katika malezi ya watoto kwa kuhakikisha wanapata
huduma na malezi bora ambayo yatawezesha kuongeza kasi ya mafanikio katika
malezi na makuzi ya awali ya watoto na hatimaye kufikia ukuaji timilifu.
Hata
hivyo kwa mujibu wa takwimu za taifa za makisio ya idadi ya watu zilizotolewa
na idara ya afya Takwimu ya Taifa.Tanzania ina takribani ya watoto 16,524,201
wavulana wakiwa 8,328,142, na wasichana 8,196,056 wenye umri kuanzia 0 -8 ambao
ni 30% ya watu wote .
Comments
Post a Comment