Jumla Ya Miradi 99 Ya Maendeleo Ya Kamilishwa Katika Kipindi Cha Mwaka Mmoja Mkoani Rukwa.


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mhe. Joseph Mkirikiti ametoa taarifa ya Mkoa wa Rukwa katika kipindi cha mwaka mmoja wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania uwepo wa amani na utulivu, umoja na mshikamano ambapo wananchi wa Mkoa wa Rukwa wamekuwa wakiendelea kufanya shughuli zao za kujiongezea kipato bila vikwazo vyovyote.

Akizungumza  ofisini kwake  Mkirikiti ametoa ufafanuzi katika miradi mbalimbali iliyotolewa fedha na serikali na mafanikio yaliyopatina ambapo Sekta ya Afya Katika kipindi cha mwaka mmoja mkoa umepokea shilingi Bilioni 1.3 kwaajili ya ujenzi wa vituo vya afya vitano (05) .

Sekta ya maji Mkoa umepata mafanikio makubwa katika sekta ya maji ambapo jumla ya Miradi 99 yenye thamani ya shilingi Bilioni 25.5 ilisainiwa kwa ajili ya kuanza utekelezaji ambapo kati ya hizo shilingi Bilioni 16.6 zilipokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa Miradi hiyo ya maji na tayari miradi 39 imekamilika na inatoa maji.

Kwa upande wa Sekta ya Elimu katika kipindi cha mwaka mmoja tumepokea jumla ya shilingi Bilioni 16.5 kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya elimu ya Msingi, Sekondari, Chuo cha ualimu Sumbawanga na Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima.

Katika kuhakikisha kuwa Barabara zinapitika kwa ajili ya kuinua uchumi wa wananchi wa Mkoa wa Rukwa, Serikali ya Awamu ya Sita imeendelea kujidhatiti kuhakikisha kuwa Barabara zilizopo chini ya TANROADs na TARURA zinatengenezwa na kupitika muda wote
Mkoa umepangiwa Shilingi Bilioni 15 kwa ajili ya maendeleo na matengenezo ya Barabara ambapo hadi kufikia mwezi Machi tayari tumepokea jumla ya shilingi Bilioni 12.4 kwa ajili ya matengenezo na maendeleo ya Barabara zilizo chini ya Wakala ya Barabara Tanzania

Comments