MABAHARIA 11 wa meli
ya MV.Mbayamwezi ya Burundi wameokolewa baada ya meli yao kuzama ziwa
Tanganyika ikitokea Zambia kuelekea nchini Burundi.
Akitoa taarifa kwa Waandishi wa habari jana Kamanda wa polisi mkoani Rukwa Willium Mwampagale alisema kuwa meli hiyo ya MV.Mbayamwezi yenye usajili wa namba BY 0074 mali ya Rafiki Ibrahimu chini ya kampuni ya Red marine ya Burundi ilizama ziwa Tanganyika katika maeneo ya Kabwe wilayani Nkasi mkoani Rukwa baada ya kupigwa na dhoruba kali februari 17 majira ya saa 5 asubuhi.
Alisema kuwa Meli hiyo
ilitoka Mpulungu nchini Zambia kuelekea Nchini Burundi tarehe 16 ya
mwezi huu ikiwa ibebeba malighafi ya kutengenezea saruji ikiwa na Mabaaria 11
ambapo Wakongomani ni 6,Warundi 5 na Mtanzania 1 ndipo kesho yake walipofika
eneo la Kabwe wilayani Nkasi walikumbana na dhoruba kali iliyopelekea meli hiyo
kuyumba na kuzama.
Kamanda Mwampaghale
alidai kuwa baada ya meli hiyo kuzama mabaharia hao walivaa vifaa vya
kujiokolea na walikaa majini masaa 24 hadi walipokwenda kuokolewa na
askari Polisi,JWTZ ikiwa ni pamoja na Wavuvi.
Alisema jitihada za
kuwaokoa Mabaharia hao zilizaa matunda ambapo walikimbizwa katika kituo cha
afya Kirando kwa matibabu na walipata huduma ya kwanza na kupata nafuu na hadi
sasa wanaendelea vizuri.
Capteni wa meli hiyo
Ramadhan Katambo Morris alidai kuwa baada ya meli hiyo kuzama yeye alikua
ni mtu wa kwanza kutoka ndani ya meli hiyo na kupiga mbizi huku akipiga mayowe
ya kuomba msaada ndipo wavuvi na wengineo walijitokeza kwenda kutoa msaada wa
kumuokoa na kuwaokoa wengine.
Alisema kuwa meli hiyo
yenye uwezo wa kubeba tani 18 siku hiyo ilibeba mzigo wa tani 17 na kuwa
uzito ulikua sahihi bali ni upepo tu uliwayumbisha na mwisho wa siku meli yao
ikazama
Mganga mfawidhi wa
kituo cha afya Kirando Benedict Tilamasi alikiri kuwapokea Mabaharia hao wakiwa
11 huku sita kati yao wakiwa mahututi na kuwa baada ya kuwapatia huduma ya
kwanza na kuendelea na matibabu mengine afya zao zimeendelea kuimalika.
Alisema wote sasa wapo
vizuri kiafya ambapo mmoja wao ndiyo bado afya yake haijaimarika na wanaendelea
kumpatia matibabu zaidi.
Comments
Post a Comment