Waziri Wa Maji Kuzindua Miradi Ya Maji Katika Vijiji Vya Sopa Na Katete Wilayani Kalambo Disember 17/2021
Waziri wa Maji
Mheshimiwa Jumaa Aweso (Mb) anatarajia kufanya ziara ya kikazi ya siku mbili
kwenye wilaya za Sumbawanga, Kalambo na Nkasi kuzindua na kuweka mawe ya msingi
kwenye miradi ya maji vijijini.
Kwa mujibu wa
taarifa iliyotolewa na Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Denis Bandisa imesema Waziri
Aweso ataanza ziara hiyo tarehe 17 na 18 mwezi huu ambapo atazindua miradi
miwili ya maji kijiji cha Kizungu, Sopa na Kitete wilaya ya Kalambo.
Katika siku ya
pili ya ziara yake atakagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maji ya
kijiji cha Kirando na Kisura wilaya ya Nkasi.
Pamoja na shughuli
zingine Waziri Aweso atapata fursa ya kuongea na wananchi kwenye maeneo yote ya
miradi wakati wa ziara yake mkoani Rukwa.
Kwa upande wake
Meneja wa Wakala wa Usambazaji Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA)
mkoa wa Rukwa Mhandisi Pius Boaz alisema maandalizi ya ziara hiyo yamekamilika
na kuwa wananchi wajitokeze kwenye maeneo ya miradi ili wamsikilize Waziri
atakapozindua miradi na kuongeza na wananchi.
Comments
Post a Comment