Halmashauri za mkoa wa Rukwa zimetakiwa kuhakikisha miradi ya ujenzi wa vyumba vya madarasa kwenye shule za sekondari na msingi chini ya Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 yanakamilika ifikapo Desemba mwaka huu.
“Maelekezo
yangu ni kuwa tupo nyuma ya ratiba ya utekelezaji miradi hii hivyo nataka
Wakurugenzi wa Halmashauri zote kuongeza kasi ya usimamizi na ufuatiliaji ili
fedha zilizotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan zipate matokeo tarajiwa kabla ya
Desemba 15 madarasa yote yawe yamekamilika kujengwa” alisema Mkirikiti.
Akiwa kwenye ziara ya kukagua miradi ya elimu na afya kwenye Halmasahauri ya wilaya ya Kalambo na Sumbawanga , Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti aliagiza Wakurugenzi kuhakikisha miradi hiyo inakamilika pasipo visingizio kwa kuwa fedha tayari zipo kwenye akaunti zao tangu mwezi Octoba mwaka huu.
Mkirikiti
aliongeza kusema, katika kutekeleza miradi hiyo ya ujenzi ni budi halmashauri
zikazingatia matumizi sahihi ya fedha kwa kuwa na miradi bora na endelevu
ambapo msisitizo vifaa kama saruji, mbao na mabati vinunuliwe kwa kuzingatia
bei ya soko.
Aliongeza
kusisitiza ushirikishwaji wa kamati za ujenzi kwa kila mradi kulingana na
Mwongozo ulitolewa na Ofisi ya Rais Tamisemi ambapo wananchi wanatakiwa
kutambua na kushiriki kwenye miradi hii.
Kupitia
Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano dhidi ya UVIKO-19 Mkoa wa
Rukwa ulipokea jumla ya shilingi 8,940,000,000 ambapo kati hizo shilingi
6,800,000,000 zitatumika kwa ajili ya ujenzi wa madarasa 332 ya shule za
sekondari na madarasa 74 kwenye vituo shikizi pamoja na mabweni ya walemavu.
“Jumla
ya madarasa 259 kwa shule za sekondari yenye thamani ya shilingi 5,180,000,000,
vyumba vya madarasa katika vituo shikizi vya shule za msingi 73 yenye thamani
ya shilingi 1,460,000,000 na mabweni mawili kwa ajili ya wanafunzi wenye
ulemavu yenye thamani ya shilingi 160,000,000 yatajengwa kupitia mradi huu
kwenye mkoa wa Rukwa” alisisitiza Mkuu wa Mkoa Mkirikiti.
Aidha,
kiasi cha shilingi 2,140,000,000 kati Bilioni 8.940 zitatumika kwa ajili ya sekta ya afya kwa
ajili ya ujenzi wa majengo (2) majengo ya huduma za dharura (EMD) kwa Milioni
600 na ujenzi jengo moja la huduma za wagonjwa mahututi (ICU) kwa shilingi
Milioni 100 wilaya ya Kalambo.
Kwa
mujibu wa taarifa hiyo, mkoa pia utatekeleza ununuzi mashine za Mionzi tatu (3)
(X-Ray) kwa shilingi Bilioni 1.26 na ujenzi wa nyumba mbili (2) za watumishi wa
afya Nkasi na Kalambo kwa shilingi
Milioni 180.
Comments
Post a Comment