Watoto Watakiwa Kupewa Kipaumbele Kutembelea Vivutio Vya Utalii

 Na Baraka Lusajo- Rukwa 

Wananchi kutoka vijiji 16 vinavyozunguka Maporomoko ya maji ya mto Kalambo wameanza kunufaika na uwepo wa Maporomoko hayo baada ya Serikali kuanza kufanya maboresho ya miundombinu ya barabara itakayogharimu zaidi fedha kiasi cha Shilingi milioni 132 za Kitanzania

Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Kalambo una ukubwa wa hekta 43,334 na unamilikiwa na kusimamiwa na wakala wa huduma za misitu Tanzania TFS kupitia kanda ya nyanda za juu kusini wilaya ya Kalambo.

Hifadhi hiyo ilihifadhiwa kisheria mwaka 1957 na ilipandishwa hadhi kuwa hifadhi ya mazingira Asilia mwaka 2019 baada ya kuonekana kuwa na hazina kubwa na Hifadhi hii ilihifadhiwa kisheria mwaka 1957 na kupandishwa hadhi kuwa Msitu wa kutangazwa na gazeti la serikali mwaka 2019 chini ya usimamizi wa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) ukiwa na ukubwa wa hekta 43,334.

Licha ya uwepo wa msitu huo lakini pia kuna kivutio kikubwa cha Maporomoko ya maji ya Kalambo yenye umaarufu katika bara la Afrika na duniani kote. Umaarufu wa maporomoko hayo umerekodiwa katika maandiko mbalimbali.

Maporomoko hayo yanapatikana katika Msitu wa Hifadhi ya Mazingira Asilia Kalambo uliopo wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa, Nyanda za Juu Kusini mwa Tanzania kwenye latitude 08′3″ kusini na longitude 3 7′14″ Mashariki. Hifadhi ya Mazingira Asilia ipo karibu sana na Ziwa Tanganyika katika Wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa takribani kilomita 20 kutoka maeneo husika.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanywa mwaka 1920 na kurekodiwa katika maandiko mbalimbali (Wikipedia) ilionyesha kuwa maporomoko hayo yana urefu wa meta 235 na upana wa kati ya meta 3.6-18.

Pia maporomoko hayo ni ya pili barani Afrika baada ya Maporomoko ya TUGELA yaliopo nchini Afrika kusini.

Maporomoko hayo yapo umbali wa Km 120 kutoka Sumbawanga Mjini. Kuna njia kuu tatu za usafiri ili kufikia maporomoko haya: Usafiri wa kutumia barabara: Kutoka Dar-es-Salaam- Sumbawanga – Matai. kutoka Mwanza – Sumbawanga – Matai. Pia unaweza kutuimia usafiri wa Ndege au usafiri wa maji kupitia ziwa Tanganyika

Aidha wageni kutoka Arusha, Mwanza na Dar-es- Salaam wanaweza tumia Uwanja wa ndege wa Songwe uliopo Mkoani Mbeya baada ya hapo kutumia barabara kutoka Mbeya hadi Sumbawanga Usafiri wa kutumia njia ya majini: Watalii wanaweza tumia Meli toka Manispaa Kigoma hadi bandari ya Kasanga iliyopo wilayani Kalambo 

Pia Mtalii atakapokuwa anashuka kuelekea kwenye maporomoko atapata fursa ya kupata mwonekano (View points) vilivyopewa hadhi ya majina ya viongozi muhimu Kituo cha kwanza; Proffesor Dossantos Silayo View point (baada ya mita 299.6) Kituo cha Pili; Brigedia Jenerali Mkeremmy View point (baada ya mita 239.9) Kituo cha tatu; Dr. Hamis Kigwangala View point (baada ya mita 157.5).

Awali akiongea wakati wa maadhimisho ya siku ya utalii dunia yalioenda sambamba   na utoaji zawadi za michezo katika kijiji cha mpombwe wilaya ya kalambo mkoani Rukwa ,mhifadhi mkuu wa hifadhi ya mto Kalambo Joseph Chezue ,alisema  michezo hiyo inalenga kutoa elimu kwa wananchi juu ya umuhimu wa kutembelea na kulinda vivutio vya utalii.

Alisema watoto ni kundi jingine ambalo linapaswa kupewa kipaumbele katika swala zima la kulinda na kutunza vivutio vya utalii  na kusisitiza walimu kutoa fulsa kwa watoto wa shule kutembelea vivutio vya utalii ikiwemo maporomoko ya kalambo fallse.

Comments