Wananchi
wilayani Kalambo mkoani Rukwa wameiomba serikali kulifanya zoezi la upandaji
miti kuwa ajenda ya kudumu kwa kuhakikisha kila kaya inakuwa na miti ya kutosha
ambayo itawezesha kuondokana na tatizo la maafa ambayo yamekuwa yakijitikeza na
kusababisha baadhi ya watoto wa shule kupata shida kutokana majengo ya shule
kuezuliwa na upepo kwa baadhi ya maeneo.
Wameyasema hayo kupitia maadhimisho ya maafa duniani ambayo kimkoa yamefanyika katika kijiji cha Matai ‘’B’’ Wilayani humo na kusisistiza serikali kusisitiza swala la upandaji miti kwenye maeneo ya taasisis ikiwemo shule ili kuwalinda watoto wa shule na majanga hayo.
Awali akiongea kupitia maadhimisho hayo mkuu wa
wilaya hiyo Tano Mwela ,alisema kwa halmshauri ya Kalambo mwaka 2020/2021 jumla
ya kaya 245 zilipoteza makazi kutokana na maafa na kwa mwaka huo huo maafa
yalisababisha vifo vya watu wawili.
Alisema
katika kushughulikia changamoto hizo wilaya itahakikisha inawatumia wataalam wa
ujenzi wa maendeleo ya jamii,watendaji wa vijiji katika kutoa elimu ya jinsi ya
kufuata taratibu za ujenzi ili kuepuka maafa.
Comments
Post a Comment