Watu 36 Wakiwemo Askari Watatu Wa SUMAJKT Wanashikiliwa Na Jeshi La Polisi Kwa Tuhuma Za Mauaji Na Uwizi Wa Pikipiki.

 Na Baraka Lusajo- Rukwa.

Jeshi la polisi mkoani Rukwa limeripoti matukio matatu tofauti likiwemo la watu 36 wakiwemo askari watatu wa SUMA JKT ambao ni walinzi wa chuo cha udaktari cha Bakhita wilayani Nkasi baada ya kuhusika na tuhuma za mauaji kwa kumpiga na lungu mtu aliyedaiwa kuwa ni mwizi kisha kusababisha kifo chake hapo papo.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoani humo ACP William Mwampagale amesema katika tukio la kwanza wanawashikilia watu watano wakiwemo askari watatu wa SUMA JKT kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mtu aliyedaiwa kuwa ni mwizi.


‘’Tulifanikiwa kuwakamata watuhumiwa watano kati yao wakiwemo askari watatu wa SUMA JKT ambao ni walinzi wa chuo cha taaluma ya udaktari wa tiba kiitwacho Bakhita kilichopo wilaya ya Nkasi kwa kosa la kumpiga na kusababisha kifo cha mtuhumiwa ambaye walimkamata kwa kosa la wizi. Mtuhumiwa atafikishwa mahakamani muda wowote upelelezi utakapokamilika.’’alisema kamanda Mwampagale.

Alisema katika tukio lingine wanawashikiria watu 31 wakiwa na pikipiki 21 ambazo umiliki wake ni wa mashaka.

Alisema kati ya hao watuhu


miwa watatu wametiwa hatiani na kufungwa jela na watuhumiwa wengine watafikishwa mahakamani muda wowote pindi upelelezi utakapo kamilika

‘’Pia katika tukio jingine tumefanikiwa kuwakamata watuhumiwa sugu wa uvunjaji kwenye mikoa ya jirani na hapa kwetu wakiwa na Kompyuta mpakato 2 aina ya Sumsung Chrome na moja aina ya HP, Printer moja,Mashine ya kupigia mapigo ya moyo na begi mbili ndogo vyote mali ya Jerone Longe raia wa Marekani’’alisema kamanda Mwampagale.

Licha ya hilo aliwataka wananchi mkoani humo kuendelea kushirikiana na jeshi la polisi kwa kutoa taarifa za uhalifu ili kuzuia matukio ya uhalifu wa aina zote.

Comments