VIJIJI VYA SINGIWE NA CHARAMINWE KUONDOKANA NA ADHA YA MAJI


Na Baraka Lusajo - Kalambo

Mwenge wa uhuru umetembelea na kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo wilayani Kalambo ikiwemo mradi wa ujenzi wa miundombinu ya mradi wa maji Singiwe unaogharimu fedha kiasi cha shilingi million 265,263,744.07

Akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi huo meneja wa RUWASA wilayani humo Patrick Ndimbo amesema mradi huo unatarajia kuhudumia wakazi 5,968 kutoka vijiji vya Singiwe na Charaminwe

Alisema katika kuhakikisha mradi huo unakuwa endelevu wilaya kupitia RUWASA imeunda na kusajili kikundi cha watoa huduma ya maji ngazi ya jamii (CBWSO) kilicho sajiliwa kwa jina la NZWALO ambacho kinasimamia shughuli za uendeshaji na matengenezo ya mradi huo


Awali akizindua mradi huo kiongozi wa mbio maalumu za mwenge wa uhuru Luten Josephine Mwampashi,aliwataka wananchi kuendelea kuulinda mradi huo ili uweze kudumu  kwa muda mrefu

Comments

  1. Duh safi sana mkuu kwa kutufikishia taarifa moja kwa moja ndani ya wilaya yetu!

    ReplyDelete

Post a Comment