Ahukumiwa Kwenda Jela Miaka 31 Kwa Kosa La Kubaka Na Shambulio La Kudhuru Mwili*

Mahakama ya wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa imemhukumu Ibrahimu moses mkazi wa kijiji cha Kisumba mwenye umri wa Miaka 26 kutumikia kifungo cha miaka 31 jela kwa kosa la kumbaka mwanafunzi  mwenye umri wa miaka 15.

Akisoma shitaka hilo mbele ya Hakimu Mkazi wa mahakama ya wilaya hiyo NCKSON TEMU, mwendesha mashitaka wa jeshi la polisi Rajabu Ndunda  amesema mshitakiwa alishitakiwa kwa kosa la kubaka na kumshambulia  mwanafunzi kinyume cha sheria na kwamba mshitakiwa alitenda kosa hilo machi 9,2020  kwa kumwingilia kimwili bila ridhaa yake.

 Wakati wa ungamo,mshitakiwa aliiomba mahakama isimpe adhabu kali kwani hilo ni kosa lake la kwanza na pia anafamilia inamtegemea .yenye mke na mtoto mmoja.

Mwendesha mashitaka hakuwa na kumbukumbu za nyuma za mshitakiwa  na aliiomba mahakama impe adhabu kali mtuhumiwa ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia chafu na ovu kama hiyo.

Awali, akisoma hukumu hiyo hakimu wa mahakama ya wilaya hiyo  Nikison Tem , amesema  mshitakiwa alitenda kosa hilo kinyume na  sheria kifungu cha  130  na (2)(e) cha kanuni ya adhabu sura ya 16  mapitio ya  mwaka 2019 pamoja na kifungu cha  shambulio la kudhuru mwili kifungu cha  241 cha  kanuni ya adhabu sura  na ya 16 ya mapitio sheria ya mwaka 2019.

Aidha kwa kuzingatia utetezi wa mshitakiwa na maombi ya Mwendesha mashitaka,Hakimu alimhukumu mshitakiwa  kwenda jela miaka 30 kwa kosa la kubaka huku kosa la kushambulia mwili akihukumiwa mwaka mmoja na kufanya jumla ya miaka 31.

Comments