Na baraka lusajo - Rukwa
Jeshi la polisi mkoani Rukwa limeanzisha utaratibu maalumu wa kuwatambua watumaji wa barabara kwa kutoa mafunzo na kuwatunuku vyeti watumiaji wa vyombo vyote ikiwa ni jitihada za kupunguza ajali zembe na makosa ya barabarani ambayo yamekuwa yakijitokeza na kugharimu maisha ya watu.
Akiongea
wakati wa kufunga mafunzo ya usalama barabarani yaliojumuisha madereva kutoka
wilaya tatu za mkoa wa Rukwa ,Kamanda wa jeshila la polisi mkoani humo ACP Wiliam Mwampagale, alisema ajali
zimekuwa chanzo cha madhara ya kifamilia ,kijamii na kitaifa na kubainisha kuwa watu wengi
wamekuwa wakipata ulemavu wa kudumu na
watoto kuachwa yatima kutokana na awepo wa ajali.
‘’zigatieni sheria kanuni na alama za barabarani ilikupunguza ajali zembe (zingatieni utii wa sheria bila shuruti) ‘’alisema Mwampagale.’’
Aidha
aliwasisistiza madereva wa magari kuhakikisha wanakagua vyombo vyao mara kwa
mara kwa kufunga mikanda wawapo kwenye vyombo vyao na kusistiza kutoendesha vyo
vya moto kwa mazoea.
Kwa
upande wake mkurugenzi wa taasisi ya shule ya usalama barabarani (GACIOUS DRIVING SCHOOL.GDS TANZANIA. Alisema
changamoto za uwepo wa ajari zimekuwa zikisababisha watoto kuachwa yatima
kutokana na wazazi au walezi kufariki kwa ajali.
Comments
Post a Comment