Bodi ya Bonde la maji ya ziwa Tanganyika imezuia kuendelezwa kwa ujenzi wa makazi ya wananchi kandokando ya ziwa Tanganyika na kupiga malufuku wakandarasi kuendesha shughuli za ujenzi wa miradi mikubwa ya serikali kwenye maeneo ya ziwa bila kuwa na vibali vya matumizi ya maji kutoka kwenye mamlaka husika.
Ziwa Tanganyika lina
urefu wa km 673 na upana wa km72 huku eneo lote likiwa na km2 za
eneo 32,900 na ujazo wa km3 18,800 huku urefu wa ufukwe ukiwa ni km
1,828.
Licha ya hilo ziwa
Tanganyika limezungukwa na nchi ya Tanzania, kongo, Burundi na Zambia huku
wananchi kutoka sehemu zote za nchi hizo wakilitegemea katika shughuli za uvuvi
na usafiri.
Licha ya uwepo wa
ziwa hilo lakini bado kumekuwa na changamoto ya mabadiliko ya tabia ya nchi,
ambapo kwa mwaka 2020 /2021 kumekuwa na mabadiliko ya kupwa na kujaa kwa ziwa
hilo na kusababisha madhara kwa wananchi pamoja na serikali kuingia hasara
kubwa kutokana na miradi yake kuharibika.
Hata hivyo kuongezeka kwa ziwa Tanganyika
kumesababisha bodi ya maji ya ziwa Tanganyika kutembelea maeneo yote yalioathiriwa
na maji ili kuona madhara kwa ujumla.
Akiongea wakati wa
kutembelea bandari ya Kasanga pamoja na soko la samaki Kasanga, Mwenyekiti
wa bodi ya maji ya ziwa Tanganyika Juliusi Shilungushela, alisema bodi hiyo
ilitembelea maeneo yote ya mwambao wa Ziwa Tanganyika ili kuona madhara kisha
kutoa ushauri wa kukabiliana na Ongezeko la maji hayo.
Kwa
upande wake Ogamba Koneli kutoka ofisi za bonde la maji ya ziwa Tanganyika,
alisema bodi imeazimia kuweka alama katika maeneo yote yanayozunguka ziwa hilo
ili kusaidia wananchi kutofanya ujenzi pindi maji yanapo kuwa yakipungua.
Hata
hivyo hivi karibuni Mkurugezni Mtendaji wa Halmashauri ya Kalambo Msongela Palela,
alitembelea maeneo yote yaliotengwa na wananchi wa vijiji vya Kasanga na
Kilewani kwa ajili ya ujenzi wa soko jipya la samaki baada ya soko la awali
kuzingilwa na maji ya ziwa Tanganyika.
Hata
hivyo Mkurugenzi huyo alibainisha kuwa serikali imetenga fedha kiasi cha shilingi
million 150 kwa ajili ya kusaidia ujenzi wa soko hilo na kubainisha kuwa
million 78 zimetengwa na wizara ili kusadia kazi hiyo.
Comments
Post a Comment