Na Baraka Lusajo - Rukwa
Shirika
linalo husika na utetezi wa mzingira nchini LEAT limeadhimisha siku ya
mazingira dunia kwa kuendesha michezo pamoja na kukabidhi vifaa mbalimbali vya
michezo kwa watoto wa shule za msingi katika bonde la ziwa Rukwa wilaya ya Sumbawanga
mkoani Rukwa.
Siku
hii inayoadhimishwa ulimwenguni kila mwaka na ilianza zaidi miaka 40 iliyopita
na huvuma Zaidi kwenye mitandao ya kijamii.
Maadhimisho
ya Siku ya Mazingira Duniani yamepanuka na kuwa jukwaa la kimataifa la
kuhamasisha na kuchukua hatua kuhusu masuala nyeti ya mazingira kuanzia kwa
uchafuzi baharini, ongezeko lajoto duniani hadi kwa matumizi ya bidhaa kwa njia
endelevu na uhalifu dhidi ya wanyamapori.
Hata hivyo Mamilioni ya watu wameshiriki katika
miaka iliyopita, na kuleta mabadiliko jinsi tunavyotumia bidhaa na kwenye sera
za mazingira za kitaifa na kimataifa.
Tangu
mwaka wa 1974, imekuwa ikiadhimishwa kila mwaka tarehe 5 mwezi wa Juni ikileta
pamoja serikali, mashirika ya biashara na wananchi kushughulikia masuala nyeti
yanayoathiri mazingira.
Hata hivyo kwa mkoa wa Rukwa maadhimisho hayo
yaliadhimishwa kwa njia tofauti tofauti, ambapo katika bonde la ziwa Rukwa shirika
la LEAT liliadhimisha maadhimisho hayo
kwa kutoa elimu kwa wananchi pamoja
na kugawa vifaa vya michezo kwa watoto
wa shule.
Mkurugezni
wa shirika hilo Kelvini Swai alisema Siku ya Mazingira Duniani ni jukwa la
kimataifa la kuleta mabadiliko chanya. Huhimiza watu binafsi kutafakari kuhusu
kile wanachokila kwa mashirika ya biashara kubuni mifumo isiyochafua mazingira
kwa wakulima na makampuni
Alisema
siku hiyo huzingatia Zaidi uzalishaji kuzalisha kwa njia endelevu kwa serikali
kuwekeza kwenye uboreshaji wa mazingira kwa taasisi za elimu kuelimisha
wanafunzi kuchukua hatua na kwa vijana kujenga hatima isiyochafua mazingira.
Alisema
shirika hilo lina hakikisha watoto wanakuwa msitari wa mbele katika kuboresha
mazingira yao.
Hata
hivyo katika wilaya ya Kalambo maadhimisho hayo yaliadhimishwa kwa kutoa elimu
kwa wafugaji kuhakikisha wanatoa lishe ya maziwa kwa watoto wenye umri chini ya
miaka 5 .
Kaimu
mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Wilbroad Kansapab, alisema wafugaji wanawajibu
wa kutunza mazingira kwa kuacha kupitisha mifugo kwenye vyanzo vya maji pamoja
na kuto kata miti hovyo.
Alisema
wagaji wanawajibu wa kuhakikisha wanawapeleka watoto wao shule badara ya kuwapeleka machungoni.
Comments
Post a Comment