Jeshi
la Polisi la mkoani Rukwa linawashikilia watu watano kwa kujihusisha na matukio
ya kiuharifu ikiwemo matumizi ya siraha kinyume na utaratubu.
Katika
operesheni iliofanyika wilayani Kalambo Jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mtu
mmoja baada ya kupatikana na siraha moja aina ya Pisto iliokuwa imetengenezwa
kienyeji na kwamba siraha hiyo ilikuwa ikitumika katika shughuli za uwindaji
haramu.
Hata
hivyo katika Operesheni hiyo Jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mtu mmoja huko
katika eneo la Reginamundi lililopo kata ya Izia Tarafa ya Lwiche manispaa ya Sumbawanga
akiwa na kete 3 za Bhangi.
Kwa
mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Rukwa Kamishna Msaidizi wa polisi Wiliam
Mwampagale,alisema licha ya hilo katika Manispaa hiyo walifanikiwa kumkamata
mtu mmoja akiwa na noti mbili za bandia
.
Mbali
na hilo Kamanda Mwampagale alisisitiza kuwa Jeshi hilo limeendelea na Operesheni
hiyo maalumu na kufanya ukaguzi wa
Magari 915 ambayo kati ya hayo Magari 574 yalionekana kuwa ni mazima, magari
333 yalionekana ni mabovu na jumla ya
magari 8 yaliondolewa namba kwa kukosa
sifa za kutembea barabarani.
‘’jumla
ya madereva 732 walichukuliwa hatua mbalimbali za kisheria ikiwa ni pamoja na
kutozwa faini na kiasi cha shilingi 21,960,000/= kilikusanywa kutokana na
makosa hayo.
Comments
Post a Comment