Jamii yatakiwa kuwalinda watoto dhidi ya matukio ya ukatili

Na Baraka Lusajo - Rukwa

JAMII Mkoani Rukwa imetakiwa kuendelea kupinga na kukemea matukio ya ukatili wa kijinsia dhidi ya watoto kutokana na makosa hayo wilayani kalambo kuongezeka kutoka matukio 27 kwa mwaka 2020 hadi kufikia makosa 37 kwa mwaka 2021 sawa na asilimia 0.45 huku watu 12 katika kipindi cha miezi mitano wakihukumiwa kifungo cha maisha jela kutokana na tuhuma za ubakaji wa watoto.

Akiongea kupitia maadhimisho ya
mtoto wa Afrika ambayo Kimkoa yamefanyikia wilayani Kalambo mkoani Rukwa mratibu wa dawati la jinsia na watoto wilayani humo Anna Kimbe, Alisema

“Kwa kipindi cha miezi mitano mwaka 2021 ambapo jumla ya makosa 32 yaliyo ripotiwa ukilinganisha na miezi mitano mwaka 2020 ambapo makosa yaliyoripotiwa hii ni sawa na ongozeko la makosa 5 ambayo ni sawa na silimia 0.45’’.  Alisema Kimbe

Alisema makosa ya ukatili wa kijinsia yaliongezeka baada ya elimu kutolewa na kusababisha jamii kutambua umihimu wa kutoa taarifa kwenye vyombo vya dola.


‘’Makosa ya ukatili yameongezeka baada ya elimu kutolewa kwa jamii hivyo jamii kutambua umuhimu wa kutoa taarifa za malalamiko hayo kituo cha polisi kwa wakati tofauti na kipindi cha nyuma kabla ya elimu kuifikia jamii,ambapo hata walipotendewa ukatili walimaliza majumbani kwao, alisema Kimbe.

Mkuu wa wilaya hiyo kalorius misungwi ambae alikuwa ni mgeni Rasmi kwenye maadhimisho hayo alisema wananchi wanawajibu wa kuendelea kuwalinda watoto dhidi ya matukio ya ukatili.

Comments