Na mwandishi wetu - Nkasi
Mkuu wa wilaya Nkasi mkoani Rukwa Peter Lijualikali amewafuta Kazi askari Mgambo watatu wa kijiji cha Swahila kata ya Mkwamba ikiwa ni pamoja na kumvua madaraka kaimu afisa mtendaji wa kijiji hicho kwa kosa la kuunda genge la uhalifu kupitia ofisi ya serikali ya kijiji kwa kuwabambikiza kesi Wananchi na kuwatoza faini kinyume cha sheria ikiwa ni pamoja na kutoa adhabu ya viboko kwa watuhumiwa wa Makosa mbalimbali.
Uamuzi huo
umetolewa jana kwenye mkutano wa hadhara baada ya mkuu huyo wa wilaya kupokea
kero kutoka kwa Wananchi wa kijiji hicho ambapo wamesema kuwa kijiji hicho
wameunda baraza la kijiji la kimila ambalo limejitungia sheria kinyume cha
sheria na iliyopelekea kunyanyasika wananchi kwa kupewa tuhuma na kuwekwa
mahabusu na kupigwa faini Kuanzia Tshs, 300,000 hadi milioni 1 ili kuachiwa.
Mmoja
wa Wananchi hao Jellad Boniface alisema mbele ya mkuu wa wilaya kuwa yeye
alipata adhabu ya kupigwa fimbo na kaimu afisa mtendaji wa kijiji hicho Yohana
Simbeye na kupigwa faini ya Tshs, 400,000 kwa kosa la kuzozana na mkewe
nyumbani kwao na kuwa wameshitakiwa na Jamhuri kwa kosa hilo na alilipa faini hiyo
bila hata ya kupewa Risiti.
Redemita
Anset alisema kuwa mmewe alikamatwa kwa kosa la kulima bangi na alipotaka
kuthibitishiwa kosa hilo alionyeshwa picha ya shamba hilo kwenye Simu hivyo
hakutakiwa kujitetea ndipo alipopewa adhabu ya kupigwa fimbo na askari Mgambo
na kulazimika kulipa faini ya Tshs, 600, 000.
Wananchi waliweza kutoa malalamiko mengi na
kubwa la kuchapwa viboko wakiwemo Wanawake ambao walikua wakikutwa na Makosa
mbalimbali na kwa wale wasiokuwa na fedha ya kulipa faini na Wana mifugo
nyumbani kwao ofisi ya kijiji utafuta wateja wa mifugo yao na kuiuza ili
watuhumiwa waweze kuachiwa kutoka katika mahabusu ya kijiji.
Kufuatia
hari hiyo mkuu wa wilaya Peter Lijualikali aliamua kuwafukuza Kazi askari
Mgambo watatu wa kijiji hicho ambao ni Robert Tito, Kulwa Madeni na Serina
Kambaulaya na kumvua madaraka ya kukaimu Uafisa mtendaji wa kijiji Yohana
Simbeye huku mwenyekiti wa kijiji hicho Gefrin George akikabidhiwa kwa
mwenyekiti wa CCM wa wilaya Salum Sudi kwa kumchukulia hatua za kididhamu ikiwa
ni pamoja na kumvua uanachama kwa kosa la kuunda genge la uhalifu katika ofisi
yake na kutengeneza sheria ndogo ambazo hazijapitishwa na halmashauri na
kuwakandamiza Wananchi.
>
Kaimu mkurugenzi mtendaji wa wilaya Asubisye Rajae alisema kuwa kutokana na
malalamiko hayo aliyoyasikia toka kwa Wananchi atawachukulia hatua za kinidhamu
Watumishi wake waliohusika katika vitendo hivyo viovu ambao ni kaimu afisa
mtendaji wa kijiji hicho ambaye pia ni afisa kilimo wa kata na afisa mtendaji
wa kata hiyo kwa kosa la kushindwa kuwajibika na kuruhusu vitendo haramu kufanyika
kwenye ofisi ya serikali.
Naye mwenyekiti wa CCM wilaya Salum Sudi
alidai kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimefedheheshwa Sana kwa kitendo cha
mwenyekiti wa kijiji anayetokana na CCM kujiingiza kwenye vitendo vya
kuwakandamiza Wananchi na kufanya uonevu hadharani na kuwa Chama kitachukua
hatua za haraka dhidi yake.
Uongozi wa kijiji cha Swahila umekuwa
ukilalamikiwa na Wananchi kwa kipindi kirefu ndipo mkuu huyo wa wilaya
Alipoamua kwenda katika Kijiji hicho ili kuweza kupata ukweli wa malalamiko
hayo na kuweza kubaini uovu mkubwa unaofanya na ofisi ya serikali ya kuwanyanyasa
Wananchi
Comments
Post a Comment