Serikali
mkoani Rukwa kwa kushirikiana na taasisi ya utafiti wa wa kilimo {TARI} na mashirika
mengine nchini, imezindua mpango mkakati wa upimaji tathimini ya udongo mradi unaotarajiwa
kuwafikia wakulima wapatao 4000 katika vijji 400 kupitia wilaya tatu za mkoa
huo kabla ya mwaka 2021 kuisha.
Mradi
huo ni mwendelezo wa awamu ya kwanza iliyozinduliwa mwaka 2019 na kuwafikia
wakulima na wadau wa kilimo wapatao 20,000 katika mikoa miwili ya Njombe na
Songwe.
Awali akiongea wakati wa uzinduzi wa mradi huo, kaimu mkuu wa mkoa wa Rukwa Kalorius Misungwi,alisema mradi huo unatarajiwa kuhudumia wakulima 4000 katika vijiji 400 .
Alisema
kupitia mradi huo wakulima wataweza kuinua vipato vyao kwa kulima kilimo chenye
tija, na kupitia mradi huo mazao ya wakulima yataongezeka maradufu.
Mkurugezi
mtendaji wa kampuni ya OCP Tanzania Dkt Mshindo Msolla, alisema kampuni yake
inashirikina na Serikali kuandaa mchakato wa upimaji wa udongo kwa zaidi ya
vijiji 100 ndani ya mkoa wa Rukwa
Alisema
lengo kubwa ni kuwaelimisha wakulima juu ya udongo wa eneo lao bila gharama
zozote, na kusisitiza kuwa majibu yatatolewa kwa wakulimu muda mfupi baada ya
vipimo kufanyika.
‘’mradi
huu wa upimaji udongo unatarajiwa kuendeshwa katika vijiji 400 na kuwafikia
wakulima wapatao 4000 kufikia mwisho wa mwaka 2021. Mradi huo pia unatarajiwa kutoa
mapendekezo ya mbolea kwa wakulima wapatao 14000 watakao wakilisha wakulima
wenzao kutoka mashamba mbalimbali, kwa kutumia njia rahisi za upimaji udongo ili
kupata matokeo sahihi.’’ Alisema Msolla.
Mradi
wa upimaji tathimini unaoratibiwa kwa ushirikiano wa Serikali ya Jamhuri ya Mungano
wa Tanzania kupitia Wizara ya kilimo , pamoja na Taasisi ya utafiti wa kilimo
TARI.
Comments
Post a Comment