Wafanyakazi Mkoani Rukwa watakiwa kupinga ajira za watoto wadogo majumbani

 Na Baraka lusajo  - Rukwa


Katika maadhimisho ya siku ya wafanyakazi duniani nchini Tanzania Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amesema licha ya matamanio yake ya kuongeza mishahara lakini inamuwia vigumu kufanya hivyo kwa sasa.

 

 "Ndugu zangu mimi ni mama na mama ni mlezi ila kuna msemo usemao kuwa masikini huwa anapenda mwanae apendeze lakini shida ni uwezo."

 

Rais Samia amesema ameshindwa kutimiza matamanio ya wafanyakazi mwaka huu kwa kuwa kasi ya uchumi imeshuka na kwa Tanzania uchumi umeshuka kutoka asilimia 6.9 mpaka asilimia 4.7 na hii inatokana na mlipuko wa janga la corona.

 

Lakini amehaidi kupunguza kodi na tozo mbalimbali za serikali kwa wafanyakazi. Aidha imemuwia vigumu kuongeza mshahara kwa kuwa ndio kwanza anaanza kazi lakini mwakani ataweza kutimiza dai hilo ambalo ni mhimu kwa wafanyakazi.

 

Kwa kutambua umuhimu wa wafanyakazi amesema wanaenda kupandisha vyeo vya wafanyakazi 85,000 mpaka 91,000 ambao wataigharimu serikali milioni, wanakusudia kulipa malimbikizo ya mishahara, kuboresha miundo ya kiutumishi na kuongeza ajira mpya takribani elfu arobaini.

 


Vilevile wataongeza jitihada za kudhibiti mfumko wa bei za bidhaa, hivyo anatumaini kwa jitihada hizo zitasaidia maisha ya watanzania.

 Kwa sekta ya umma na sekta binafsi zinapandisha kima cha chini cha mshahara na kuagiza kuundwa mara moja kwa bodi ya mishahara itakayomwezesha kufahamu kiwango cha kuongeza katika mishahara ya watumishi wa umma na sekta binafsi.


Hata hivyo wafanyakazi mkoani Rukwa wameungana na watu wengine dunia kote katika kuadhimisha siku ya wafantakazi ambayo imefanyika kimkoa katika wilaya ya Kalambo.

Katika maadhimisho hayo shirikisho la vyama huru vya wafanyakazi Tanzania TUCTA  kupitia risala limebainisha kuwa linaamini katika ushirikiano wa pamoja  na mahusiano mema ndio ustawi wa taasisi zetu na nchi kwa ujumla na kwamba wote wanapaswa kuzingatia utawala wa sheria kwa kuzifuata ipasavyo ili itendeke kwa wanyakazi  na vyama vingine.

Hali kadharika wafanyakazi mkoani humo walisistizwa kuwa msitari wa mbele katika kupinga na kukemea ajira za watoto  majumbani .

Comments