TASAF AWAMU YA TATU KUWASADIA WATOTO WANAO KOSA MILO MITATU KWA SIKU.

 Na Baraka lusajo  - Rukwa 

Halmashauri ya Kalambo Mkoani Rukwa imeanza utekelezaji wa kuibua kaya masikini katika vijiji 45 ambavyo vilikuwa vimesalia katika awamu ya kwanza ya utekelezaji wa mpango huo huku ikijidhatiti kuondoa wanufaika hewa kwa kuweka mfumo rafiki wa malipo  ikiwa ni pamoja na kuangalia familia zenye watoto waliokosa misaada.


Katika kipindi cha kwanza, vijiji na mitaa 9,960 sawa na 70% vilifikiwa , ambapo jumla ya kaya milioni 1.36 zilitambuliwa na kati ya hizo kaya milioni 1.1 zenye jumla ya watu milioni 5.4 ziliandikishwa kwenye masijala ya walengwa.

Hata hivyo katika kipindi cha pili cha awamu ya tatu ya mfuko wa maendeleo ya jamii TASAF, kilizinduliwa rasmi, februali 17-2020 huku kipindi cha pili awamu ya tatu ya TASAF (PSSN 11) kilianza kutekelezwa mwaka 2020 hadi mwaka 2023 ambapo wilaya 184 za Tanzania bara na visiwani ikiwemo Unguja na Pemba ziliingizwa kwenye mfumo huo.


Hata hivyo kwa wilaya ya Kalambo mpango huo umelenga kuvifikia vijiji 45 ambavyo vilikuwa vimesalia katika awamu iliyopita, ambapo Halmashauri imeunda timu za wasimamizi na wawezeshaji wa zoezi hilo katika vijiji hivyo.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo Msongela Palela amebainisha kuwa zoezi la utambuzi wa kaya utafanywa na wanajamii kupitia mikutano ya vijij/Mitaa kwa usimamizi wa wawezeshaji kutoka kwenye mamlaka za maeneo husika.

Aidha Msongela alibainisha kuwa walengwa watakuwa ni kaya zinazoishi katika mazingira duni na hatarishi.

alisema licha ya hilo mpango utalenga kuwezesha kaya za walengwa kutumia furisa za kuongeza kipato ,huduma za jamii na kiuchumi na kuwekeza katika maendeleo ya watoto ambao ni rasilimali watu.

Alisema mpango huo utajikita zaidi kuwasaidia watoto wenye umri  wa kwenda shule ambao wamekosa milo mitatu kwa siku  na wanaoishi kwenye mazingira hatarishi.

alisema licha ya hilo mpango huo utajikita zaidi katika kuwasaidia watoto ambao hawaendi  kiliniki kupata huduma za afya .


“Vigezo vya kaya za walengwa ni kaya ambazo zinakipato cha chini si cha uhakika ukilinganisha na kaya zingine katika kijiji au mtaa, pia zitaangaliwa Zaidi kaya ambazo hazimudu au hazina uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku pamoja na familia zenye makazi duni. Alisema Msongela’’

Kwa upande wake kaimu mkurugenzi mkuu wa Mfuko wa kunusuru Kaya masikini TASAF nchini Beatrice Shemdoe,alisema kipindi cha pili awamu ya Tatu ya Mfuko wa maendeleo ya jamii (TASAF II) kinatekelezwa katika Halmashauri 184 za Tanzania bara na visiwani na kubainisha kuwa kipindi hiki kitafikia zaidi ya wananchi milioni moja nchini kote.

“Mkazo mkubwa katika kipindi chapili umewekwa katika kuziwezesha kaya masikini ili kuziongezea kipato’’ alisema Shemdowe.

Alisema walengwa watakao tambuliwa na kuandikishwa katika kipindi cha pili ni kaya zinazoishi katika hali duni kwenye vijiji, mitaa na shehia na kwamba wanufaika ndani ya kaya watakuwa ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano wanao hudhuria kliniki.


Mkuu wa wilaya hiyo Kalorius Misungwi aliwasisitiza watendaji kuwa waadilifu wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo na kuwasisitiza kufanya kazi kwa bidii kwa malengo ya kupunguza umasikini na kuchochea ukuaji wa uchumi ukiwemo ule wa viwanda ambayo ni ajenda muhimu ya serikali.

“Nitoe ushauri kwa viongozi wenzangu, tunapofanya ziara zetu za kikazi katika maeneo yetu tutenge muda wa kuongea na walengwa na kuwahamasisha kuanzisha miradi ya ujasiriamali ili kukuza vipato vya kaya zao na kuwa na akiba ya kujikimu ili hata pale ruzuku inapochelewa au kusitishwa wawe wamejiwekea misingi bora. Alisema Misungwi.

 

Comments