Ujenzi huo utagharimu dola za Marekani bilioni 3.55, na unatarajiwa kuwa mradi wenye bomba refu zaidi la mafuta dunian
Maafikiano ya
mwisho ya mradi huo - na wafadhili wa ujenzi huu- utaafikiwa na mataifa haya
mawili na makampuni ya mafuta kabla ya ujenzi huo haujaanza.
Mataifa haya mawili yanatarajia kukuza uchumi na kuzalisha ajira
zipatazo 10, 000 wakati wa ujenzi wa bomba hilo na uendeshaji wa mradi huo.
Uganda
inakadiriwa kutoa mapipa yake ya kwanza ya wastani wa bilioni 1. 4 ya mafuta
yanayofaa kibiashara mnamo 2025.
Rais Samia
pamoja na mwenyeji wake Rais Museveni, amehudhuria hafla na utiaji saini
mkataba kati ya Serikali ya Uganda na Kampuni ya Mafuta Ghafi ya Afrika
Mashariki (EACOP) juu ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta
ghafi la kutoka Hoima nchini Uganda kwenda Tanga nchini Tanzania.
Rais Samia amealikwa Ikulu ya Entebbe na mwenyeji wake Rais
Yoweri Museveni na kuanza kukaguwa gwaride la heshima liloandaliwa kwa ajili
yake.
Baada ya kukaguwa gwaride Museveni na mgeni wake walifanya
mkutano wa faragha pamoja na kampuni ya Total baada ya hapo watasaini
utekelezaji wa ujenzi wa bomba la mafuta la mradi mkubwa wa dhamani ya dolla
bilioni 15.
Hii ni safari ya kwanza kwa rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania
tangu kuchukua madaraka baada ya kifo cha Hayati Dkt John Pombe Magufuli.
Mwaka 2020, aliyekuwa rais wa Tanzania Hayati John Pombe
Magufuli na Rais Yoweri Museveni walisaini makubaliano ya jenzi wa bomba hilo
unaogharimu dola za Marekani bilioni 3.5.
Ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Hoima -Tanga wenye
urefu wa jumla ya Kilometa 1,443 zikiwemo 1,115 zitakazojengwa ndani ya ardhi
ya Tanzania utagharimu dola za Marekani bilioni 3.55, unatarajiwa kusafirisha
mapipa laki 2 ya mafuta kwa siku na wakati wa ujenzi unatarajiwa kuzalisha
ajira kati ya 6,000 na 10,000.
Comments
Post a Comment