Tanzania na Uganda wasaini mkataba wa ujenzi wa bomba la mafuta

Ujenzi huo utagharimu dola za Marekani bilioni 3.55, na unatarajiwa kuwa mradi wenye bomba refu zaidi la mafuta dunian


Maafikiano ya mwisho ya mradi huo - na wafadhili wa ujenzi huu- utaafikiwa na mataifa haya mawili na makampuni ya mafuta kabla ya ujenzi huo haujaanza.

 

Mataifa haya mawili yanatarajia kukuza uchumi na kuzalisha ajira zipatazo 10, 000 wakati wa ujenzi wa bomba hilo na uendeshaji wa mradi huo.

Uganda inakadiriwa kutoa mapipa yake ya kwanza ya wastani wa bilioni 1. 4 ya mafuta yanayofaa kibiashara mnamo 2025.

 


Rais Samia pamoja na mwenyeji wake Rais Museveni, amehudhuria hafla na utiaji saini mkataba kati ya Serikali ya Uganda na Kampuni ya Mafuta Ghafi ya Afrika Mashariki (EACOP) juu ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la kutoka Hoima nchini Uganda kwenda Tanga nchini Tanzania.

 

Rais Samia amealikwa Ikulu ya Entebbe na mwenyeji wake Rais Yoweri Museveni na kuanza kukaguwa gwaride la heshima liloandaliwa kwa ajili yake.

 

Baada ya kukaguwa gwaride Museveni na mgeni wake walifanya mkutano wa faragha pamoja na kampuni ya Total baada ya hapo watasaini utekelezaji wa ujenzi wa bomba la mafuta la mradi mkubwa wa dhamani ya dolla bilioni 15.

 

Hii ni safari ya kwanza kwa rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania tangu kuchukua madaraka baada ya kifo cha Hayati Dkt John Pombe Magufuli.

 

Mwaka 2020, aliyekuwa rais wa Tanzania Hayati John Pombe Magufuli na Rais Yoweri Museveni walisaini makubaliano ya jenzi wa bomba hilo unaogharimu dola za Marekani bilioni 3.5.

 

Ujenzi wa mradi wa bomba la mafuta ghafi la Hoima -Tanga wenye urefu wa jumla ya Kilometa 1,443 zikiwemo 1,115 zitakazojengwa ndani ya ardhi ya Tanzania utagharimu dola za Marekani bilioni 3.55, unatarajiwa kusafirisha mapipa laki 2 ya mafuta kwa siku na wakati wa ujenzi unatarajiwa kuzalisha ajira kati ya 6,000 na 10,000.

Comments