Rais Samia ataka uhuru wa vyombo vya habari uheshimiwe

Rais wa Tanzania Bi.Samia Suluhu Hassan amesema ni muhimu kusimamia vyombo vya habari vya ndani.


Rais Samia amesema "nasikia kuna vyombo vya habari vilivyofungiwa fungiwa na TV za mikono, vifungulieni na vifuate sheria na muongozo wa serikali".

Aliongeza kusisitiza kuwa ;"Tusiwape mdomo wa kusema kuwa tunaminya uhuru wa vyombo habari."

Aidha Rais Samia amesema wahakikishe kuwa kila atakayepewa ruhusa ya kuendesha chombo cha habari anafuata sheria za serikali na kanuni ziwe wazi kuwa kosa ili adhabu yake ilingane na adhabu inayotolewa.

"Tusifungie tu kibabe, wafungulieni lakini hakikisha wanafuata miongozo ya serikali".

Comments