Rais wa Tanzania Bi.Samia Suluhu Hassan amesema ni muhimu kusimamia vyombo vya habari vya ndani.
Rais Samia
amesema "nasikia kuna vyombo vya habari vilivyofungiwa fungiwa na TV za
mikono, vifungulieni na vifuate sheria na muongozo wa serikali".
Aliongeza
kusisitiza kuwa ;"Tusiwape mdomo wa kusema kuwa tunaminya uhuru wa vyombo
habari."
Aidha Rais
Samia amesema wahakikishe kuwa kila atakayepewa ruhusa ya kuendesha chombo cha
habari anafuata sheria za serikali na kanuni ziwe wazi kuwa kosa ili adhabu
yake ilingane na adhabu inayotolewa.
"Tusifungie
tu kibabe, wafungulieni lakini hakikisha wanafuata miongozo ya serikali".
Comments
Post a Comment