Ujenzi wa vyumba 5 katika shule ya sekondari Mambwe wa kamilika''Kalambo''

 



Halmashauari ya Kalambo mkoani Rukwa imefainikiwa kukamilisha ujenzi wa vyumba 5 vya madarasa katika shule ya Sekondari Mambwe iliyopo katika kata ya Ulumi na kuwawezesha wanafunzi 240 waliokuwa wamekosa nafasi kuendelea na masomo yao.

Shule ya sekondari Mambwe ilianzishwa rasmi mwaka 1995 kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza na cha nne,  ambapo mpaka hivi ssa ina jumala ya wanafunzi 650  kwa kidato cha kwanza hadi cha nne  ikiwemo wavulana 372 na wasichana 278. Pia inawanafunzi 180 wa kidato cha tano na cha sita.

Afisa elimu Sekondari wilayani humo Jeshi Lupembe, alisema shule hiyo kabla ya ujenzi wa madarasa matano shule ilikuwa na vyumba vya madarasa kumi na sita kati mahitaji ya vyumba vya madarasa 20 na kufanya kuwa na upungufu wa vyumba vya madarasa 4.

’Shule hii inapokea wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne kutoka kata mbili ikiwemo kata ya Ulumi na Kata ya Mnamba ambayo haina shule ya sekondari ‘’Alisema lupembe.

Kaimu afisa mipango wilayani humo Emily Mwakalinga, alisema katika ujenzi huo, Halmashauri ili changia vifaa vya ujenzi (saruji,mabao  ,nondo,miusumari ,rangi,whiti sement na bati) pamoja na kulipia gharama za ufundi  na usafiri  na kughalimu  fedha kiasi cha shilingi 40,35,000.00.

Awali akikagua ukamilishwaji wa miradi ya ujenzi wa shule hiyo katibu mkuu wa jumuiya ya serikali za mitaa (ALAT) Elirehema Kahoyo, aliwataka wananchi kuendelea kujitolea nguvu zao na kuipongeza Hamashauri kwa kufanikiwa kutoa miti 300 ya miti ya matunda na mbao kwa kila shule.

Aidha, alisisitiza shule zote kuweka mkakati wa kuanza kuvuna maji ya mvua kwa kuweka matenki ili kuwawezesha wanafunzi kutokukosa huduma ya maji

Comments