
Bw. Mabeyo amemhakikishia
kuwa ulinzi wa nchi na mipaka yake ni salama na vitaendelea kumlinda, kumtii
kama Amirijeshi mkuu na kutekelezamajukumu yake kwa mujibu wa katiba ya
Tanzania.
‘’Tunakuahidi utiifu,
uadilifu na uaminifu mkubwa kama ilivyo ada ya mila na desturi ya majeshi yetu
katika awamu zote zilizopita kwa manufaa ya ulinzi, usalama na ujenzi wa taifa
letu’’. Alisema Jenerali Mabeyo.
Jenerali Mabeyo alisema
hayo mjini Chato wakati akimpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuapishwa kuwa
Amirijeshi Mkuu.
Kuhusu namna
alivyomfahamu na kufanya naye kazi hayati Magufuli Jenerali Mabeyo alisema;
‘’Aliviamini na kuvipenda
vyombo vya ulinzi na usalama alihakikisha kuwa anaviwezesha kwa mahitaji ya
kiutendaji na utawala ili viweze kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi na weledi
mkubwa.’’
‘’Alisema hatuwezi kuwa
na vyombo vya ulinzi imara bila kuwa na uchumi madhubuti, hatuwezi kutegemea
misaada ya kuimarisha vyombo vyetu lazima tuimarishe uchumi wetu ili tuweze
kuimarisha vyombo vyetu vya ulinzi na usalama.’’
Mabeyo amesema
walishiriki katika kulinda mgodi wa Tanzanite, na kulinda, kujenga ukuta kuzunguka mgodi huo.
Hata hivyo kwa upande wake Rais wa
awamu ya nne wa Tanzania Jakaya Kikwete amesema taarifa ya kifo ilikuwa jambo
gumu kulipokea na kulikubali.
Akieleza
mahusiano yake na hayati Magufuli tangu alipokuwa waziri wake, Kikwete amesema
alikuwa jembe lake.
Nilipokuwa
Rais, Magufuli alikuwa Waziri wangu kwa miaka 10, alikuwa mmoja wa mawaziri
niliowaamini na kumtumaini.
‘’Alikuwa
jembe langu ndio maana nilimuweka kwenye wizara tatu zilizokuwa ngumu ili
anyooshe mambo.’’ Alisema Kikwete.
‘’Yalikuwa
matumaini yangu na matarajio yangu angemaliza kipindi chake cha uongozi salama,
akastaafu na kuishi maisha marefu baada ya hapo na kupata nafasi ya kutuzika
sisi watangulizi wake ambao ni kaka zake, hili la kututoka kabla ya kumaliza
muhula wake na sisi kumzika yeye ni jambo ambalo sikuwahi kulifikiria kabisa.’’
Alisema Kikwete.
Amesema
uongozi wake bado ulikuwa ukihitajika Tanzania, na kuwa alikuwa akitamani
akamilishe kazi yake nzuri aliyokwisha ianza.
Comments
Post a Comment