Hayati Rais Magufuli azikwa Chato


Ni safari ya mwisho ya Hayati Rais John Pombe Magufuli , amelazwa katika nyumba yake ya milele.

Amezikwa kwa taratibu zote za kijeshi ambazo anapaswa kupatiwa Amiri Jeshi Mkuu.

Mizinga 21 imepigwa ikiashiria heshima kubwa kwa kiongozi huyu.

Hayati Magufuli amezikwa katika eneo la makaburi ya familia mjini chato , mkoani geita.

Watu wa karibu na familia pamoja na viongozi ndio wameshiriki moja kwa moja katika mazishi haya kwa kufika Geita na wengine kufuatilia moja kwa moja kwenye matangazo ya Televisheni.

Comments