Rais Magufuli Ametahadharisha Kuhusu Matumizi Ya Dawa Za Kupambana Na Covid-19 Zinazotoka Nje

 

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli amewataka watanzania kutumia dawa za asili katika mapambano dhidi ya Covid-19

Akizungumza Jijini Dodoma hii leo, amesisita juu ya matumizi ya miti shamba pia kujifukiza katika mapambano dhidi ya Covid-19.

Aidha amesema kuwa si kila dawa zinazotoka nje ya nchi ni nzuri kwa watanzania.

''Kuna dawa inaitwa Covidol, Bugiji zinafanya kazi kwasababu zimekua proved na mkemia mkuu, kamwe msifikirie kila dawa inayotoka nje ni kwa ajili yenu, ingekua hivyo Malaria ingeisha. Tujitambue tusitumike. Madawa haya yalipigwa vita na wakoloni kwasababu ya uchumi, ukiwa na mti wako hata kama unaponesha malaria utaambiwa ni wa kishamba''. Alisema Magufuli

Ameitaka pia Wizara ya Afya kutoa ushirikiano kwa wagunduzi wa dawa za asili.

''Mungu ametupatia hii mimea na ikabarikiwa, tuitumie, lakini tuitumie kwa kufuata masharti na utaalamu mzuri, kwa hiyo Taasisi yetu ya Wizara ya Afya inayosimamia dawa za asili, huu ni wakati wa kuyatumia kikamilifu. Na Wizara ya Afya isiwakatishe tamaa watu hawa, na madaktari wanatumia hizo hizo dawa, wao wanaenda wanakunywa, wanajifukiza wakija huku wanawatwanga masindano'' Alisema.

Ameongeza pia kuwa Watanzania kwa wakati wote wamemtanguliza Mungu na kuendelea kujilinda hivyo wanapaswa kuendelea kuchukua tahadhari.

Viongozi wa ngazi mbalimbali pia wameendelea kuhamasisha matumizi ya dawa asili katika mapambano ya Covid-19.

 

Comments