Na baraka lusajo- Kalambo
Daraja
la Kale lililopo katika kata ya Ulumi linalounganisha vijiji 11 vya kata 3 za
wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa limesombwa na maji kufuatia mvua kubwa
ilionyesha katika maeneo hayo na kusababisha kukatika kwa mawasiliano ya
barabara.
Wananchi katika maeneo hayo wamesema daraja hilo linaunganisha vijiji 11 kutoka kata za Ulumi,Mambwekenya na Mnamba na kuelezea kuwa ili kuyafikia maeneo hayo ni lazima upitie na kuvuka kwenye daraja hilo na kuiomba serikali kuharakisha ujenzi wa daraja hilo.
Meneja wa TANROAD mkoani Rukwa Mhandis Mgeni Mwanga
, alisema serikali imeanza jitihada za kuusafisha mto huo na kuweka mawe lengo
likiwa ni kuweka kivuko cha muda wakati wakisubiri bajeti ya daraja kubwa
kujengwa kwenye mto huo.
Comments
Post a Comment