Na Israel
Mwaisaka,Nkasi
KATIBU wa afya wa
halmashauri ya wilaya Nkasi Ibrahimu Kashatila (29) amefariki dunia baada ya
kutumbukia kwenye kisima kilichopo mjini Namanyere.
Kwa mujibu wa taarifa
iliyotolewa na kaimu kamanda wa Polisi mkoani Rukwa Theopista Mallya ni
kuwa taarifa za kupotea kwa marehemu zilitolewa na mkewe January 23,2021 na
juhudi za kumtafuta ziliendelea na ndipo January 27 majira ya saa 11:30 jioni
zilitolewa taarifa za mwili wa kijana huyo kupatikana kwenye kisima akiwa
amekufa.
Amesema kuwa marehemu
alitoka nyumbani kwake januari 23 ya mwaka huu akienda matembezini na kuwa toka
siku hiyo hakuonekana nyumbani wala kazini kwake na taarifa zilitolewa Polisi
na juhudi za kumtafuta ziliendelea hadi pale mwili wake ulipopatikana kwenye
kisima kilicho karibu na bar moja mjini Namanyere inakosadikika kuwa
alikua wakinywa pombe na ulipatikana baada ya siku 4.
Kamanda Mallya alisema
kuwa uchunguzi wa jeshi la Polisi unaendelea ili kuweza kubaini chanzo cha kifo
hicho na kuwa wao kama Polisi kwa sasa wanasubiri taarifa ya kitabibu ambayo
wataiunganisha na taarifa za kiuchunguzi.
Alisema kuwa
sasa ni mapema sana kwao kuzungumza mambo kwa kina lakini uchunguzi
ukikamilika watatoa taarifa nzima ya tukio hilo.
Ndugu wa
marehemu walikabidhiwa mwili kwa ajiri ya mazishi baada ya hatua za
awali za uchunguzi kukamilika
Mwisho
Comments
Post a Comment