Dkt Abbas:Tanzania inazingatia tahadhari dhidi ya corona

 


Msemaji mkuu wa serikali nchini Tanzania Dkt. Hassan Abbas amesema Tanzania inazingatia miongozo yote ya tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona na hata wakati huu ambao dunia inapambana na wimbi la pili la maambukizi ya virusi hivyo.

Akihojiwa na kitoa cha redio cha EFM kilichopo jijini Dar es salam, Dkt. Abbas amesema “Sisi Tanzania msimamo wetu ni ule ule,tunafahamu tatizo lipo duniani na dunia inahangaika lakini cha kwanza watanzania waondoe hofu wizara ya afya ilishatoa miongozo, ile miongozo bado ipo haijawahi kufutwa kuna tahadhari za kuchukua hivi wewe kunawa mikono mpaka covid? Alihoji Dkt Abbas.

‘’ Tulikuwa tuna nawa sana shule baadaye tukaacha kwahiyo kuna zile tahadhari kama alivyosema juzi Mh Rais tuendelee kuzichukua lakini Tanzania tunaamini tumedhibiti haya maambukizi kwa njia zetu za kisayansi na kumshukuru Mwenyezi Mungu’’.

‘’Unajua Tanzania watu wanasahau wanafikiri tulidharau sana huu ugonjwa tulichukua hatua zote dunia ilizokuwa inataka isipokuwa kujifungia ndani maana kuna watu wanatamani sana kufungiwa ndani sijui kuna nini huko ndani” Alisema Bw. Abbas.

Comments