Na Zillipa Joseph -Katavi
Ongezeko
la watumishi wa idara ya afya mkoani Katavi limeelezwa kuleta mafanikio katika
utoaji wa huduma mbalimbali hususan huduma za mama na mtoto
Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi baadhi ya wananchi wa
vijiji vya Ugalla, Kambuzi na Kabage katika Halmshauri ya Nsimbo Wilaya ya
Mpanda mkoani Katavi wamesema kwa sasa wakifika hospitali wanahudumiwa haraka
na kuondoka
Bi. Maria Malendeka ni mkazi wa kijiji cha Kanoge anaeleza kuwa
awali kinamama wenye watoto walilazimika kushinda siku nzima wakisubiri huduma
katika zahanati ya Ugalla
“Ulikuwa unakuja hapa zahanati asubuhi ni mpaka jioni kabisa
ndio unaondoka lakini sasa wahudumu wameongezeka ukikaa sana ni masaa mawili
matatu” alisema Maria
Awali zahanati hiyo ilikuwa inahudumia vijiji vitatu Ugalla,
Kambuzi na Kabage na ilikuwa na wahudumu watatu tofauti na sasa ambapo ina
wahudumu watano
“Watoto walikuwa wanalia njaa kwa kukaa muda mrefu bila kula,
unawadanganya na machungwa au muhogo lakini sasa ukiamua unakuja hapa au
unakwenda Kanoge” aliongeza Maria
Bwana Pius Ndaji mkazi wa kijiji cha Kambuzi ameishukuru
serikali kwa kujenga hospitali za wilaya na kuongeza watumishi
Bwana Apolinari Mushi ni Katibu wa Afya mkoa wa Katavi amesema
wana ongezeko la watumishi 180 wa kada mbalimbali ambapo kwa mwaka 2018
walikuwa na watumishi 713 na sasa wana watumishi 893
Mushi amesema sanjari na ongezeko la watumishi wa idara ya afya
pia kuna ongezeko la zahanati katika vijiji mbalimbali, vituo vya afya na
hospitali
Ameongeza kuwa mwaka 2015 mkoa ulikuwa na jumla ya vituo vya
afya 79 na hadi kufikia juni 2020 kuna vituo vya afya 101 ikiwa ni ongezeko la
vituo 22
Aidha kuna Hospitali 1 ya Rufaa ya Mkoa, Hospitali 3 za
Halmashauri, na Zahanati 80 kati ya 65 zilikuzowepo
Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi Dk. Omari Sukari amesema
ongezeko hilo limeleta ufanisi mkubwa katika utoaji wa huduma za afya
Amesema kundi kubwa lililokuwa likiteseka lilikuwa ni la watoto
wa kuanzia miaka sifuri hadi nane kwani ni kundi ambalo huwezi kulikosa wakati
wowote unapofika katika sehemu za kutolea huduma za afya
“Hata vijiji ambavyo vimejenga zahanati vimesaidia kupunguza
msongamano sehemu moja” alisema Dk. Sukari
“Hizi hospitali za wilaya nazo zimesaidia watu kuacha kuja mjini
kutegemea hospitali moja kule wanapata huduma na maisha yanaendelea” aliongeza
Dk. Sukari
Comments
Post a Comment