Na zilipa Joseph –katavi
Matokeo
ya mitihani ya kupima uelewa kwa wanafunzi wa darasa la kwanza hadi la tatu
katika manispaa ya Mpanda mkoani Katavi yanaridhisha ambapo wanafunzi wamefaulu
kwa wastani wa alama 68
Afisa Elimu Msingi wa Manispaa ya Mpanda Boniface Kalulu amesema
matokeo hayo ni ya mitihani ya kufunga muhula wa pili
Akizungumzia changamoto ya ufundishaji wa
madarasa hayo kufuatia shule kufungwa kwa miezi mitatu mwaka huu kutokana na
janga la ugonjwa wa korona Kalulu amesema walimu walipata kazi ya kuanza upya
kwani watoto walio wengi hasa wa madarsa ya awali na darasa la kwanza walikuwa
wamesahau hata kuandika
Hata hivyo amesema kuwa kutokana na ubongo
wa watoto kuwa mwepesi watoto hawakukawia kurudisha kumbukumbu na masomo
yaliendelea kama kawaida
“Unajua mtoto hana mambo mengi kama mtu
mzima yeye akishika jambo ameshika” alisema
Aidha ametoa pongezi kwa walimu kwa kutia
bidii katia kazi yao hali iliyopelekea matokeo mazuri
‘Cha kushanganza mwaka uliopita wanafunzi
wa madarasa haya walifaulu kwa wastani wa asilimia 55 lakini pamoja na kucheza
kipindi ambacho tulifunga kwa ajili ya korona wamefaulu zaidi’ alieleza
Kwa upande wake mwalimu Paskali Katona
anayefundisha darasa la kwanza na la pili katika shuke ya Msingi Kashato
iliyopo katika Manispaa ya Mpanda amesema uelewa wa wanafunzi uko vizuri hali
iliyopelekea kupata matokeo mazuri
‘Katika madarasa yangu wanafunzi wengi
wamefaulu vizuri ni wachache sana ndio maksi haziridhishi lakini hao ni wale
kushika nafasi ya mwisho kila mara’ alisema mwl Katona
Baadhi ya wazazi waliofika katika shule ya msingi katavi
kuchukua ripoti za watoto wao wameonyesha kuridhishwa na matokeo
Amefanya vizuri, mwaka jana alikuwa wa 21 kati ya watoto 54 lakini
mwaka huu mwanangu amekuwa wa 14 kati ya watoto 52’ alisema Marsha Abdala
mzazi wa Shakila Ali mwanafunzi wa darasa la pili shule ya msingi Katavi
Akieleza jitihada alizofanya kama mzazi kumsaidia mtoto
kitaaluma Bi Marsha alikiri kutomsaidia mwanawe katika masomo
Kiukweli nisiongope nafasi ya kumsaidia sina sanasana
niwashukuru walimu wao ndio wamefanya kazi yote’ alisema
Wanafunzi wa shule za msingi wanamaliza muhula wa pili wa masomo
na kufunga shule hii leo na kuanza likizo ya takriban wiki tatu ambapo shule
zitafunguliwa tarehe 11 Januari 2021
Comments
Post a Comment